Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ampa miezi miwili kuanzia leo Mkurugenzi
wa Halmashauri ya wilaya ya Songwe, Elias Nawera abadili mwenendo wake
kiutendaji na ashirikiane vizuri na Mkuu wa wilaya hiyo Samwel Jeremiah
Waziri Mkuu ametoa agizo hilo Alhamisi hii, wakati akizungumza na
watumishi wa wilaya ya Songwe akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani
Songwe.
Amesema watumishi wote wanatakiwa kufanya kazi kwa ushirikiano ili
malengo ya Serikali ya kuwahudumia wananchi yaweze kufikiwa. Pia
waheshimiane sehemu za kazi na kila mtu azingatie mipaka ya madaraka
yake.
“Mkurugenzi hapa hamsikilizi Mkuu wa wilaya anaondoka kituo cha kazi
bila ya kuaga na amewagawa wakuu wa Idara. Namtaka afanye mabadiliko ya
utendaji wake ndani ya miezi miwili na Mkuu wa Mkoa fuatilia jambo
hili,” alisisitiza Waziri Majaliwa.
Pia amewaagiza Wakuu wa Wilaya wote wasimamie utendaji wa wakurugenzi
wa Halmashauri kwenye maeneo yao ili kuhakikisha wananchi wanahudumiwa
ipasavyo.”Serikali hii si ya mchezo. Serikali hii inahitaji watumishi
waadilifu wa kuwatumikia Watanzania.”
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Bibi Chiku Galawa amesema
wamejipanga kuhakikisha changamoto zote zinazoukabili mkoa zinaboreshwa
pamoja na kufikia malengo ifikapo 2020
Friday, July 21, 2017

Man United waichakaza Man City bila huruma
Klabu ya soka ya Manchester United imeendeleza ushindi katika mechi zake za kirafiki huko nchini Marekani
United ambao walikuwa wakicheza na majirani zao Manchester City asubuhi hii katika mechi ya kirafiki ya kombe la International Champions Cup 2017 mjini Houston, imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.
Magoli hayo ya Man United yaliyofungwa na Romelu Lukaku dakika ya 37 na Marcus Rashford dakika ya 39.
United ambao walikuwa wakicheza na majirani zao Manchester City asubuhi hii katika mechi ya kirafiki ya kombe la International Champions Cup 2017 mjini Houston, imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.
Magoli hayo ya Man United yaliyofungwa na Romelu Lukaku dakika ya 37 na Marcus Rashford dakika ya 39.

Picha: Diamond na mama yake walivyowasili kwenye msiba wa mama yake Zari
Msanii Diamond Platnumz pamoja na mama yake mzazi Bi Sandra wamefanikiwa
kuhudhuria katika msiba wa mama yake Zari The Bosslady nchini Uganda.
Bosi huyo wa WCB amewasili jana katika msiba huo ambao kwa mujibu wa taarifa aliyoitoa Zari kupitia mtandao wa Instagram, marehemu alifariki asubuhi ya siku ya jana (Alhamisi). Babu Tale naye ameambatana na Diamond katika msiba huo.
Bosi huyo wa WCB amewasili jana katika msiba huo ambao kwa mujibu wa taarifa aliyoitoa Zari kupitia mtandao wa Instagram, marehemu alifariki asubuhi ya siku ya jana (Alhamisi). Babu Tale naye ameambatana na Diamond katika msiba huo.

Harmorapa azidi kumganda Amber Lulu
Licha ya ukaribu wao kuchukuliwa kama kiki, msanii Harmorapa amezidi
kusisitiza yupo katika mahusiano ya kimapenzi na video vixen Amber Lulu
licha ya mrembo huyo kuwahi kukanusha hilo
Harmorapa ambaye amekuwa akivutia watu wengi kwa vituko vyake, ameiambia Boys Boys ya TV1 kuwa yeye kama kijana wa kiume ni lazima awepo katika mahusiano.
“Unajua siku zote kama ni mwanaume, halafu mwanaume rijali ni lazima uwe kwenye mahusiano ya kimapenzi, kwa hiyo mimi nina mpenzi, kuoa bado hata mtoto sina. Kwa sasa ni mtu famous, nilishamtaja ili kuna wengine hawamfahamu ni Amber Lulu,” amesema Harmorapa.
Harmorapa ambaye amekuwa akivutia watu wengi kwa vituko vyake, ameiambia Boys Boys ya TV1 kuwa yeye kama kijana wa kiume ni lazima awepo katika mahusiano.
“Unajua siku zote kama ni mwanaume, halafu mwanaume rijali ni lazima uwe kwenye mahusiano ya kimapenzi, kwa hiyo mimi nina mpenzi, kuoa bado hata mtoto sina. Kwa sasa ni mtu famous, nilishamtaja ili kuna wengine hawamfahamu ni Amber Lulu,” amesema Harmorapa.
Saturday, July 1, 2017

Jacob Zuma na makamu wake walazimishwa kusalimiana
Aliyekuwa mke wa rias wa kwanza wa Afrika Kusini Nelson Mandela,
Winnie
Madikizela Mandela aliwalazimisha viongozi wawili maaruf nchini humo
rais Jacob Zuma na makamu wa rais Cyril Ramaphosa kusalimiana.Wawili hao walikuwa katika mkutano wa chama cha ANC mjini Johannesburg.
Bwana Ramaphosa anataka kumrithi rais Zuma na amekuwa akimkashifu rais huyo kwa uhusiano wake na familia ya Gupta.
Mojawapo ya mambo yaliyobainika katika barua pepe zilizotajwa kuwa 'Guptaleaks', ni kwamba rais Zuma alikuwa amepanga kwenda kuishi katika miliki za Kiarabu UAE.
Madai ambayo yamekanwa.
Mengine yalionyesha kuwa familia hiyo ya Gupta imekuwa na ushawishi mkubwa serikalini.

Trump: Tumechoka kuivumilia Korea Kaskazini
Rais wa Marekani Donald Trump anasema muda wa uvumilivu wa kimikakati kwa Korea Kaskazini umekamilika sasa.
Katika
hotuba ya pamoja na rais wa Korea Kusini Moon Jae, kwenye ikulu ya
White house, Trump amesema kwamba vitisho vya Korea Kaskazini vinafaa
kupata majibu ya kijasiri.Hata hivyo, Trump amesema ni muhimu kuwe na ushirikiano katika kugawana mzigo wa kuhakikisha
usalama.
Rais wa Korea Kusini amesema kwamba taifa lake litaweka marekebisho ya kiuslama na kujenga msingi dhabiti wa kujikinga.
Rais Moon pia amesema ni muhimu kuendelea na majadiliano na viongozi wa Korea Kaskazini.
Kwengineko, Bwana Moon alisema kuwa ni muhimu kuendelea kujadiliana na viongozi wa Korea Kaskazini.
Bwana Moon alisema kuwa swala la Korea Kaskazini linafaa kupewa kipaumbele wakati wa mazungumzo akisisitiza kuwa ni usalama thabiti pekee unaoweza kuleta amani katika eneo zima la Pacific.
Akizungumza katika Ikulu ya Whitehouse, bwana Trump alisema kuwa wakati wa kuvumiliana na utawala Korea Kaskazini umefeli miaka mingi akiongezea: Kwa kweli uvumilivu huo umekwisha
Kiongozi huyo wa Marekani amesema kuwa serikali yake sasa inafanya kazi na Korea Kusini pamoja na Japan wakiwemo washirika wengine duniani kuchukua hatua kadhaa za kidiplomasia, usalama na kiuchumi ili kuwalinda washirika wake pamoja na raia wa Marekani dhidi ya janga hilo kwa jina Korea Kaskazini.

Lionel Messi alivyouaga ukapera!
Nyota wa timu ya Barcelona, Lionel Messi amefunga ndoa ya kifahari na
mpenzi wake wa utotoni Antonella Roccuzzo ambaye pia ni mzazi mwenzake
wa watoto wawili.
Ndoa hiyo imefungwa huko Rosario City nchini Argentina usiku wa
kuamkia leo huku ikuhudhuriwa na mastaa kibao wa soka kama kina Xavi,
Carles Puyol, Cesc Fabregas, Samuel Eto'o, Luis Suarez, Jordi Alba na
Sergio Busquets.
Wanasoka wengine walioudhuria harusi hiyo ni Sergio Agüero, Ezequel Lavezzi, Javier Mascherano na Angel Di Maria.
Wanasoka wengine walioudhuria harusi hiyo ni Sergio Agüero, Ezequel Lavezzi, Javier Mascherano na Angel Di Maria.

Sina hofu na ujio wa Okwi - Kessy
Beki wa Yanga Hassan Kessy amesema ujio wa mshambuliaji raia wa Uganda wa Klabu ya Simba Emmanuel Okwi haumtishi.
Kessy amesema siku zote anapenda akabane na mchezaji tegemeo wa timu pinzani kwa ajili ya kumpa ushindani ili aone upungufu wake ili aweze kuufanyia kazi.
"Naheshimu uwezo alionao Okwi lakini siyo kumuogopa na katika kuthibitisha hilo, nitaanza kumuonyesha tutakapokutana kwenye mechi ya Ngao ya Jamii," .
"Mimi na Okwi tunajuana kutokana na kuwahi kukutana katika mechi mbalimbali mimi nikiwa nachezea Mtibwa Sugar na yeye akicheza Simba, " amesema.
Kessy amesema anaamini ushindani utakuwa wa hali ya juu kutokana na kila klabu kusajili kutokana na mapungufu yaliyotokea katika msimu uliopita lakini yeye kwa upande wake anaendelea kujipanga ili kuhakikisha anafanya vizuri katika msimu ujao.
Kessy amesema siku zote anapenda akabane na mchezaji tegemeo wa timu pinzani kwa ajili ya kumpa ushindani ili aone upungufu wake ili aweze kuufanyia kazi.
"Naheshimu uwezo alionao Okwi lakini siyo kumuogopa na katika kuthibitisha hilo, nitaanza kumuonyesha tutakapokutana kwenye mechi ya Ngao ya Jamii," .
"Mimi na Okwi tunajuana kutokana na kuwahi kukutana katika mechi mbalimbali mimi nikiwa nachezea Mtibwa Sugar na yeye akicheza Simba, " amesema.
Kessy amesema anaamini ushindani utakuwa wa hali ya juu kutokana na kila klabu kusajili kutokana na mapungufu yaliyotokea katika msimu uliopita lakini yeye kwa upande wake anaendelea kujipanga ili kuhakikisha anafanya vizuri katika msimu ujao.

Spika Ndugai awaonya wabunge wanaochafua hali ya hewa bungeni
Spika wa Bunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai
amewaonya wabunge wanaochafua hali ya hewa kwa kauli za matusi na maudhi
bungeni waache mara moja kwani vitendo
hivyo ni vibaya kwa wapiga kura wao huku akiwashangaa kuwa huenda wakawa na matatizo yao binafsi yanayowasumbua.
Mhe. Ndugai amesema hayo jana mjini Dodoma baada ya kuwepo kwa baadhi ya wabunge wanaotoa kauli zisizokuwa rasmi katika vikao vya bunge bila kufikiria kwamba wanachokifanya hakina taswira nzuri kwa wapiga kura wao pamoja na Bunge.
Huku Ndugai akisema kuwa
“Unajua sisi tunaokaa hapa mezani hatuchangii kama nyinyi, kazi yetu ni kuwapa nafasi mseme, wakati mwingine zinatoka shutuma ambazo hatuna nafasi ya kubishana au kulumbana lakini wakati mwingine ni vizuri kutumia fursa hizi kusafisha baadhi ya mambo. Binadamu ni lazima uwe na staha ile ndogo tu kuwaheshimu binadamu wenzako,” akiwa amesisitiza kuwa
“Katika bunge letu kinacholeta matatizo humu ndani ni tabia na lugha, tukirekebisha hayo mawili tutaenda vizuri tu lakini najua kundi hili ni kubwa hatuwezi kuwa wote tupo sawa, nitaendelea kulisemea lakini pale kwenye ulazima tutachukua hatua,”
Hata hivyo Mh Ndugai amewaonya wabunge wanaochafua hali ya hewa bungeni kwa lugha chafu waache vitendo hivyo kwani hao ndiyo wanaoudhi kwa kauli zao za kusema bunge ni dhaifa huku akisisitiza kuwa wabunge aliowapa adhabu bado adhabu yao iko pale pale ya kukaa nje ya bunge kwa mwaka mmoja.
hivyo ni vibaya kwa wapiga kura wao huku akiwashangaa kuwa huenda wakawa na matatizo yao binafsi yanayowasumbua.
Mhe. Ndugai amesema hayo jana mjini Dodoma baada ya kuwepo kwa baadhi ya wabunge wanaotoa kauli zisizokuwa rasmi katika vikao vya bunge bila kufikiria kwamba wanachokifanya hakina taswira nzuri kwa wapiga kura wao pamoja na Bunge.
Huku Ndugai akisema kuwa
“Unajua sisi tunaokaa hapa mezani hatuchangii kama nyinyi, kazi yetu ni kuwapa nafasi mseme, wakati mwingine zinatoka shutuma ambazo hatuna nafasi ya kubishana au kulumbana lakini wakati mwingine ni vizuri kutumia fursa hizi kusafisha baadhi ya mambo. Binadamu ni lazima uwe na staha ile ndogo tu kuwaheshimu binadamu wenzako,” akiwa amesisitiza kuwa
“Katika bunge letu kinacholeta matatizo humu ndani ni tabia na lugha, tukirekebisha hayo mawili tutaenda vizuri tu lakini najua kundi hili ni kubwa hatuwezi kuwa wote tupo sawa, nitaendelea kulisemea lakini pale kwenye ulazima tutachukua hatua,”
Hata hivyo Mh Ndugai amewaonya wabunge wanaochafua hali ya hewa bungeni kwa lugha chafu waache vitendo hivyo kwani hao ndiyo wanaoudhi kwa kauli zao za kusema bunge ni dhaifa huku akisisitiza kuwa wabunge aliowapa adhabu bado adhabu yao iko pale pale ya kukaa nje ya bunge kwa mwaka mmoja.

TCRA yazitaka kampuni za simu kusitisha matangazo kwenye miito ya simu
Mamlaka ya Mawasiliano nchini Tanzania (TCRA), imewataka wamiliki wa
mitandao ya simu nchini kusitisha matangazo yanayosikika kabla ya muito
wa simu pindi mteja anapopiga simu
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA,James Kilaba ambapo amesema kuwa matangazo hayo yamekuwa kero kwa watumiaji wa mitandao ya simu nchini.
Aidha Kilaba anazitaka kampuni za simu kusitisha matangazo pindi mtu anapopiga simu kabla ya muito huku akisema matangazo hayo yamekuwa kero kwa watumiaji wa mitandao ya simu na hivyo kutoa wito kwa kampuni za simu zote kurudi katika utaratibu wa kawaida mtu anapopiga simu akutane na miito ya kawaida na si matangazo.
“Tunachoongelea ni kwamba kama mtu unapiga simu moja kwa moja ianze ringtone au yenyewe imeweka au mwenyewe umechagua lakini tunataka ianze kwenye ringtone ianze kuring kama hapatikani iseme ni busy tone moja kwa moja sio kwamba uanze utangulizi ukiisha huo ndio ije ringtone sasa hivi ndicho kinachotokea kwa baadhi ya makampuni ya simu,” alisema Kilaba.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA,James Kilaba ambapo amesema kuwa matangazo hayo yamekuwa kero kwa watumiaji wa mitandao ya simu nchini.
Aidha Kilaba anazitaka kampuni za simu kusitisha matangazo pindi mtu anapopiga simu kabla ya muito huku akisema matangazo hayo yamekuwa kero kwa watumiaji wa mitandao ya simu na hivyo kutoa wito kwa kampuni za simu zote kurudi katika utaratibu wa kawaida mtu anapopiga simu akutane na miito ya kawaida na si matangazo.
“Tunachoongelea ni kwamba kama mtu unapiga simu moja kwa moja ianze ringtone au yenyewe imeweka au mwenyewe umechagua lakini tunataka ianze kwenye ringtone ianze kuring kama hapatikani iseme ni busy tone moja kwa moja sio kwamba uanze utangulizi ukiisha huo ndio ije ringtone sasa hivi ndicho kinachotokea kwa baadhi ya makampuni ya simu,” alisema Kilaba.

Adele akatisha tamasha lake ghafla
Msanii wa muziki kutoka nchini Uingereza Adele, amelazimika kukatisha
tamasha lake la 123-date world tour kwa kile kinachodaiwa kupata madhara
katika koo lake(vocal cords).
Muimbaji huyo mwenye mashabiki lukuki amelazimika kukatisha show zake mbili zijazo baada ya show yake ya Juni 29 aliyofanya uwanja wa Wembley nchini humo. Kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram jana aliamua kuwaandikia mashabiki zake waliokuwa wakiisubiria tamasha hilo kuwa atashindwa kuendelea na tamasha kutokana na maradhi aliyonayo.
Muimbaji huyo mwenye mashabiki lukuki amelazimika kukatisha show zake mbili zijazo baada ya show yake ya Juni 29 aliyofanya uwanja wa Wembley nchini humo. Kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram jana aliamua kuwaandikia mashabiki zake waliokuwa wakiisubiria tamasha hilo kuwa atashindwa kuendelea na tamasha kutokana na maradhi aliyonayo.

Jay Z amtumbua mama yake
Albamu ya 13, ya rapper Jay Z imetoka na mojawapo ya ngoma inayopatikana
katika albamu hiyo ya 4:44 imeeleza kuwa mama yake ni mtu anayeshiriki
mapenzi ya jinsia moja.
Ngoma hiyo inayoitwa ‘Smile’ aliyomshirikisha mama yake imeweza kuthibitisha kuwa mama mzazi wa rapper huyo(Gloria Carter) kuwa ni mtu anayeshiriki mapenzi ya jinsia moja, Katika ngoma hiyo inasema kuwa “Mama had four kids, but she’s a lesbian,” he raps on the No I.D.-produced track. “Had to pretend so long, that she’s a thespian / Had to hide in the closet, so she medicate / Society’s shame and the pain was too much to take / Cried tears of joy when you fell in love / Don’t matter to me if it’s a him or her.”
Pia katika outro ya ngoma hiyo mama yake Jay amesikika akiimba kwa kusema “Living in the shadow/ Can you imagine what kind of life it is to live? In the shadows people see you as happy and free, because that’s what you want them to see. Living two lives, happy, but not free.”
Mama akazidi kutiririka “Living in the shadow feels like the safe place to be/ No harm for them, no harm for me. But life is short, and it’s time to be free. Love who you love, because life isn’t guaranteed. Smile.”
Hiyo ni baadhi ya mistari inayopatikana katika ngoma hiyo ili uweze kusikiliza kwa urefu zaidi cha msingi ni kuhakikisha unanunua albamu hiyo kupitia mtandao wa Tidal.
Ngoma hiyo inayoitwa ‘Smile’ aliyomshirikisha mama yake imeweza kuthibitisha kuwa mama mzazi wa rapper huyo(Gloria Carter) kuwa ni mtu anayeshiriki mapenzi ya jinsia moja, Katika ngoma hiyo inasema kuwa “Mama had four kids, but she’s a lesbian,” he raps on the No I.D.-produced track. “Had to pretend so long, that she’s a thespian / Had to hide in the closet, so she medicate / Society’s shame and the pain was too much to take / Cried tears of joy when you fell in love / Don’t matter to me if it’s a him or her.”
Pia katika outro ya ngoma hiyo mama yake Jay amesikika akiimba kwa kusema “Living in the shadow/ Can you imagine what kind of life it is to live? In the shadows people see you as happy and free, because that’s what you want them to see. Living two lives, happy, but not free.”
Mama akazidi kutiririka “Living in the shadow feels like the safe place to be/ No harm for them, no harm for me. But life is short, and it’s time to be free. Love who you love, because life isn’t guaranteed. Smile.”
Hiyo ni baadhi ya mistari inayopatikana katika ngoma hiyo ili uweze kusikiliza kwa urefu zaidi cha msingi ni kuhakikisha unanunua albamu hiyo kupitia mtandao wa Tidal.
Monday, June 26, 2017

Aishi:Sijasaini mkataba Simba
Mlinda mlango wa Azam FC na timu ya taifa ya Tanzania Aishi Salum
Manula, amekanusha kusaini na Klabu ya Simba huku akiongeza kuwa vipo
vilabu vingi vya hapa nchini alivyofanya navyo mazungumzo na muda
ukifika itajulikana na timu gani ataitumikia.
Aishi amekiri kuwa sasa yeye bado ni mlinda mlango wa Azam FC lakini ameshafanya nao mazungumzo na wamekubaliana kuondoka pale tu mkataba wake utakapoisha, huku akiongeza ya kuwa amepata ofa nyingi za vilabu vya ndani lakini kwa sasa bado sio muda mwafaka wa kutaja klabu atakayojiunga nayo baada ya kumalizana na Azam FC.
Aishi amekanusha yeye kusaini mkataba na klabu ya Simba
Aishi amesisitiza kuwa mpaka sasa bado hajajiunga na klabu yoyote
hapa nchini huku akiwataka mashabiki kuwa tayari kwani muda utakapofika
ataweka wazi kila kitu.
“Kuhusiana na kujiunga na klabu yoyote hapa nchini bado na sio muda mwafaka wa mimi kutaja Klabu ambayo nitaenda kujiunga nayo lakini wakae tayari wakinisubiri mkataba wangu utakapoisha Julai mwaka huu ndani ya Azam FC nitaweka wazi wapi naenda lakini kuhusiana na mkataba sio kweli na sijasaini na timu yoyote” amesema Aishi Manula
Aishi amekiri kuwa sasa yeye bado ni mlinda mlango wa Azam FC lakini ameshafanya nao mazungumzo na wamekubaliana kuondoka pale tu mkataba wake utakapoisha, huku akiongeza ya kuwa amepata ofa nyingi za vilabu vya ndani lakini kwa sasa bado sio muda mwafaka wa kutaja klabu atakayojiunga nayo baada ya kumalizana na Azam FC.
“Cha kusema kuhusiana na
suala la mimi kutoka Azam FC ilo niwahakikishie mashabiki na wapenda
Soka Watanzania kwamba ni kweli mkataba wangu utakapoisha Azam FC
nitaondoka ndani ya Azam lakini kuhusiana na ofa ni kweli kuna ofa
nyingi nimepata ndani ya nchi na tuliweza kuzungumza na hizo klabu
ambazo zinanihitaji na mazungumzo yameenda vizuri na yanaendelea vizuri
kwa ujumla” amesema Aishi Manula.
“Mimi sijasaini Simba na
nasikia kuna mkataba unaonyesha kwamba nimesaini Simba, hizo nadhani ni
watu wanajitahidi kutaka kujua au kuwathibitishia mashabiki waamini
kwamba nimesaini Simba lakini sio kweli, na kama ningekuwa nimesaini
Simba nadhani wao wenyewe wangeshanitangaza, ” amesema Aishi Manula.
“Kuhusiana na kujiunga na klabu yoyote hapa nchini bado na sio muda mwafaka wa mimi kutaja Klabu ambayo nitaenda kujiunga nayo lakini wakae tayari wakinisubiri mkataba wangu utakapoisha Julai mwaka huu ndani ya Azam FC nitaweka wazi wapi naenda lakini kuhusiana na mkataba sio kweli na sijasaini na timu yoyote” amesema Aishi Manula

Manowari ya Uingereza kuanza kufanyiwa majaribio leo
Manowari mpya ya Uingereza inatarajwa kuanza majaribio ya baharini leo.
HMS
Queen Elizabeth ndiyo meli kubwa zaidi kuwai kuundwa kwa jeshi la
wanamaji la Uingereza iliwa na uwanja wa ndege wenye ukubwa wa viwanja
vitatu vya soka.Meli hiyo ni kubwa hadi itahitaji kusubiri kushuka kwa viwango vya maji kuweza kupititia eneo la Forth bridges.
Manowari mpya ya Uingereza inatarajwa kuanza majaribio ya baharini leo.
HMS
Queen Elizabeth ndiyo meli kubwa zaidi kuwai kuundwa kwa jeshi la
wanamaji la Uingereza iliwa na uwanja wa ndege wenye ukubwa wa viwanja
vitatu vya soka.Meli hiyo ni kubwa hadi itahitaji kusubiri kushuka kwa viwango vya maji kuweza kupititia eneo la Forth bridges.

Uturuki yazuia maandamano ya wapenzi wa jinsia moja
Mamlaka nchini Uturuki imevunjilia mbali gwaride la wapenzi wa jinsia moja katika mji wa Istanbul, kwa mwaka wa tatu mfululizo.
Polisi walitumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya watu waliojaribu kushiriki gwaride hilo na kuwakamata baadhi yao.Mamlaka inasema imechukua hatua hiyo ili kuzima tishio la makundi yanayopinga serikali kutumia gwaride hilo kuzusha vurugu.
Wanaharakati wa kutetea haki ya wapenzi hao wa jinsia moja wamepuuzilia mbali madai hayo na kuongezea kuwa serikali inatumia vigezo hivyo kama sababu ya kuminya uhuru wa watu hao.
Wanamshutumu Rais Recep Tayyip Erdogan anayegemea maadili ya kiislamu
kwa kujaribu kuliendesha taifa kwa kutumia mtazamo wake binafsi juu ya
masuala fulani katika jamii.

Trump akosa kuandaa chakula cha Eid White House
Rais wa Marekani Donald Trump,
amevunja tamaduni ya karibu miaka ishirini kwa kukosa kuandaa chakula
cha jioni kuadhimisha kukamilika kwa mwezi mtukufu wa Ramadan.
Hafla hiyo inayoandaliwa katika ikulu ya White House imekuwa ikifanyika kila mwaka kutoka kipindi cha Rais Bill Clinton.Sherehe za Eid al-Fitr ndio mwisho wa mfungo wa Ramadan wakati waislamu hufunga
Alisema katika taarifa: "Kwa niaba ya watu wa Marekani na Melania ninatuma heri njema kwa waislamu wakati wanaposherehekea Eid al-Fitr.
Chakula cha kwanza cha Eid kilichoandaliwa Ikulu ya White House kiliandaliwa na Rais Thomas Jefferson mwaka 1805 kwa ujumbe kutoka Tunisia.
Sherehe hizo zilifufuliwa tena na Hillary Clinton mwaka 1996 wakati akiwa mama wa kwanza wa taifa.
Hafla hiyo ilianza kufanywa kila mwaka tangu mwaka 1999 na kuhudhuriwa na viongozi wa kiislamu mashuhuri nchini Marekani.

Wachezaji bongo tusiogope kwenda nje - Maguli
Mshambuliaji wa kimataifa anayeitumikia klabu ya Dhofar SC ya nchini
Oman, Elias Maguli amewataka vijana wa Kitanzania wanaotaka kuendeleza
vipaji vyao, nje ya nchi kujaribu pale wanapopata nafasi na sio kukata
tamaa.
Maguli
amesema, vijana wengi wamekuwa wakipata nafasi za kwenda katika
majaribio katika timu mbalimbali za nje ya nchi lakini wamekuwa
wakikatishwa tamaa na baadhi ya watu wanaowazunguka .
Maguli ameongeza kwa kuvitaka vilabu vya soka hapa nchini kuwaruhusu
wachezaji ili waweze kutumia nafasi wanazozipata nje ya nchi
"Kwanza wanapopata nafasi
waende. Hawawezi kupata taarifa kwamba kuna ubaguzi katika hiyo nchi
unayotakiwa kwenda kabla hujafika. Fika kwanza ndio ujue matatizo
yaliyopo katika hiyo nchi, na mimi nina imani kuna wachezaji wengi
wamepata nafasi lakini labda wao wanapenda kucheza hapa nchini,” amesema Elias Maguli.
“Kunawachezaji wengine
wameshapata nafasi lakini vilabu vimekuwa tatizo, kwani vilabu mara
nyingi huwa vinawakatalia wachezaji na hata kutaja dau kubwa na
ukiangalia sisi wachezaji wa hapa Tanzania katika viwango bado tupo
chini, hivyo tunapopata nafasi ni lazima kuzitumia ili kuweza kukuza
zaidi vipaji vyetu, ” alisisitiza Maguli.
Maguli amewataka wachezaji kutokuogopa changamoto katika soka kwani
changamoto wanazokutana nazo ndizo zinasaidia kuweza kuwakuza katika
soka.
“Unajua Tanzania kukiwa na
wachezaji wengi wa kimataifa ingekuwa ni faida kwani kila mchezaji
anapoitwa katika timu ya Taifa tungefanya vizuri zaidi ya hapa kwani
kila mchezaji anakuja na uwezo wake aliofundishwa kutoka katika klabu
yake, na pia tunajifunza vitu vingi katika maisha ya Soka, na tusiogope
changamoto kwani changamoto hata hapa nchini zipo na ndizo
zinazotusaidia kukua kisoka. Sasa kwa nini tuogope kwenda nje,
tunahitaji kuwa wengi wa kimataifa, ” amesema Maguli.

Mwigulu Nchemba:wanaotaka ushoga watafute nchi ya kwenda
Waziri wa Mambo ya ndani na Mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi Mkoani
Singida, Mwigulu Nchemba amefunguka na kuwataka watu wanaotaka haki za
ushoga watafute nchi ya kwenda ambayo isatoa haki hiyo lakini si
Tanzania.
Mwigulu Nchemba anasema kama kuna taasisi yoyote imesajilikuwa nchini na inafanya kampeni za haki za ushoga basi atazifutia usajili huo na watu wake kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Mbali na hilo Mwigulu Nchemba alipigia msumali kauli ya Rais dhidi ya
wanafunzi ambao watapata ujauzito wakiwa shuleni na kusema watu
wanaopinga jambo hilo wasitumie nguvu kubwa kupinga bali wajenge shule
zao wao watoe hiyo haki ya kusomesha wanafunzi wajawazito au wale ambao
tayari wamejifungua na siyo kulazimisha serikali ya Magufuli kufanya
hayo
Mwigulu Nchemba anasema kama kuna taasisi yoyote imesajilikuwa nchini na inafanya kampeni za haki za ushoga basi atazifutia usajili huo na watu wake kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
"Wanaotaka haki za ushoga
watafute tu nchi yao nyingine ambayo inaruhusu mambo hayo wakakae huko,
kama ni taasisi imesajiliwa kwenye nchi yetu tukaigundua inafanya
kampeni ya haki hizo na bahati nzuri zinasajiliwa Wizara ya Mambo ya
Ndani nitazifutia usajili wao, na kama ni raia wa Tanzania anaendesha
kampeni hizo tutamkamata na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria, na kama
si raia amekuja kwenye nchi yetu kuja kuendesha haki hizo tutampa amri
ya kuondoka ndani ya nchi yetu hatapata fursa hata ya kuchomoa chaji ya
simu kwenye soketi ya umeme" alisisitiza Mwigulu Nchemba .

Okwi atema cheche
Mshambuliaji wa zamani wa kikosi cha Simba Emmanuel Okwi ambaye jana
amerejea rasmi katika kikosi hicho baada ya kusaini mkataba wa
kuitumikia Simba amefunguka na kusema amekuja kupambana kuhakikisha kuwa
Simba inapata ubingwa na kufanya vizuri.
Okwi anasema amefurahi sana kurudi katika timu yake hiyo ya zamani ikiwa chini ya viongozi wapya ambao ambao wanaonekana na njaa ya timu yao kufanya vizuri zaidi hivyo ameahidi kushirikiana nao na kuhakikisha timu hiyo inafanya vyema.
Okwi anasema amefurahi sana kurudi katika timu yake hiyo ya zamani ikiwa chini ya viongozi wapya ambao ambao wanaonekana na njaa ya timu yao kufanya vizuri zaidi hivyo ameahidi kushirikiana nao na kuhakikisha timu hiyo inafanya vyema.
Marufuku kusafirisha chakula nje - Majaliwa
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa apiga marufuku usafirishaji wa
chakula nje ya nchi bila kibali na kuwataka wafanyabiashara kuuza
chakula kwenye maeneo yenye uhaba nchini.
Mhe. Majaliwa ametoa agizo hilo leo, wakati akihutubia Baraza la Iddi katika msikiti wa Masjid Riyadh mjini Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo amesema kuwa kuna maeneo ambayo wananchi hawakupata chakula vizuri kutokana na uhaba wa mvua hivyo wafanyabiashara wapeleke chakula kwenye maeneo hayo.
Waziri Mkuu amesema Serikali bado haijatoa kibali cha kutoa chakula nje ya nchi na kama kuna umuhimu kwa anayetaka anatakiwa akaombe ambapo kibali hicho kitahusu , kusaga kwaajili ya kusafirisha unga na siyo mahindi.
Waziri Mkuu Majaliwa amesema kuwa Serikali imepokea barua za maombi ya kupeleka chakula nchi jirani, lakini bado haijatoa ruhusa na kuonya wale watakao kamatwa wakisafirisha mahindi nje ya nchi kinyume na utaratibu, mahindi hayo yatataifishwa na kupelekwa kwenye ghala la Taifa na magari yatapelekwa polisi
Mhe. Majaliwa ametoa agizo hilo leo, wakati akihutubia Baraza la Iddi katika msikiti wa Masjid Riyadh mjini Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo amesema kuwa kuna maeneo ambayo wananchi hawakupata chakula vizuri kutokana na uhaba wa mvua hivyo wafanyabiashara wapeleke chakula kwenye maeneo hayo.
Waziri Mkuu amesema Serikali bado haijatoa kibali cha kutoa chakula nje ya nchi na kama kuna umuhimu kwa anayetaka anatakiwa akaombe ambapo kibali hicho kitahusu , kusaga kwaajili ya kusafirisha unga na siyo mahindi.
Waziri Mkuu Majaliwa amesema kuwa Serikali imepokea barua za maombi ya kupeleka chakula nchi jirani, lakini bado haijatoa ruhusa na kuonya wale watakao kamatwa wakisafirisha mahindi nje ya nchi kinyume na utaratibu, mahindi hayo yatataifishwa na kupelekwa kwenye ghala la Taifa na magari yatapelekwa polisi

Saida Karoli afunguka juu ya Darassa na Ray C
Msanii mkongwe wa muziki wa asili, Saida Karoli amewamiminia sifa kibao wasanii wa Bongo Fleva, Ray C na Darassa.
Saida ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya Orugambo, amesema hit song ya Darassa ‘Muziki’ ni vigumu kuja kushuka na kuwataka wasanii wengine hasa wa hip hop kuchukulia hilo kama somo.
“Wimbo wa Darassa utaendelea kuhit, utaendelea kuwa shule kwa waimbaji wa hip hop.
Nitapenda watumie akili alizotumia Darassa, mimi naamini wimbo wa Darassa hauwezi kushuka hata siku moja na Watanzania wengi walikuwa hawapendi muziki wa hip hop lakini Darassa kuonyesha njia kwa sababu sasa hivi hadi kwenye harusi wanaimba acha maneno weka muziki, hadi Bungeni,” Saida ameiambia Clouds FM.
Kwa upande wa Ray C Saida amesema licha ya msanii huyo kupitia matatizo mengi bado uwezo wake upo pale pale na kuna baadhi wamejaribu kumuiga ila wameshindwa.
“Kwa kweli Ray C nampenda sana kutoka moyoni tangu zamani, sauti yake ni nzuri haina mpinzania, wasichana wengi wamejaribu kuiga kuimba kama yeye, wanapenda mvuto wake na muonekano wake lakini wameshindwa,” amesema Saida na kuongeza.
“Na ukiangalia Ray C amepitia matatizo makubwa sana hapa katikati lakini napenda kumshukuru Rais Mstaafu Mheshimiwa Jakaya Kikwete alipomsaidia Ray C, na ningependa Rais wetu wa sasa, Dkt. John Magufuli afanye hivyo ili tuweze kunyanyuka sisi tuliokwama,” ameeleza Saida.
Saida ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya Orugambo, amesema hit song ya Darassa ‘Muziki’ ni vigumu kuja kushuka na kuwataka wasanii wengine hasa wa hip hop kuchukulia hilo kama somo.
“Wimbo wa Darassa utaendelea kuhit, utaendelea kuwa shule kwa waimbaji wa hip hop.
Nitapenda watumie akili alizotumia Darassa, mimi naamini wimbo wa Darassa hauwezi kushuka hata siku moja na Watanzania wengi walikuwa hawapendi muziki wa hip hop lakini Darassa kuonyesha njia kwa sababu sasa hivi hadi kwenye harusi wanaimba acha maneno weka muziki, hadi Bungeni,” Saida ameiambia Clouds FM.
Kwa upande wa Ray C Saida amesema licha ya msanii huyo kupitia matatizo mengi bado uwezo wake upo pale pale na kuna baadhi wamejaribu kumuiga ila wameshindwa.
“Kwa kweli Ray C nampenda sana kutoka moyoni tangu zamani, sauti yake ni nzuri haina mpinzania, wasichana wengi wamejaribu kuiga kuimba kama yeye, wanapenda mvuto wake na muonekano wake lakini wameshindwa,” amesema Saida na kuongeza.
“Na ukiangalia Ray C amepitia matatizo makubwa sana hapa katikati lakini napenda kumshukuru Rais Mstaafu Mheshimiwa Jakaya Kikwete alipomsaidia Ray C, na ningependa Rais wetu wa sasa, Dkt. John Magufuli afanye hivyo ili tuweze kunyanyuka sisi tuliokwama,” ameeleza Saida.

Gabo amzungumzia Kanumba na Wema Sepetu
Msanii wa Filamu Tanzania, Gabo amesema si kweli tasnia ya filamu imeshuka baada ya kifo cha Steven Kanumba.
Muigizaji huyo ameeleza kuwa watu wengi wanaamini kutokuwepo kwa Kanumba
kumedhoofisha soko la filamu za bongo movies ambae aliweza kuleta changamoto ambazo kwa
sasa hazipo.
“Sio kweli industry ipo vile vile, kwani jamaa alikuwa analeta changamoto kwa wacheza sinema wengi sana hivyo baada ya kuondoka ule ushindani ukawa umeshuka, hicho ndio kitu ambacho wanakikosa,” Gabo ameiambia Bongo Dot Home ya Times FM na kuongeza kuwa
“Lakini mimi nisema waendelee kuwa na mapenzi ya dhati ila wasisite kutoa malalamiko yao na kukosoa pale ambapo wanahisi pameenda tofauti kwa sababu changamoto za watu pekee ndio zinabadilisha.Tunajua hapo tunakosea inabidi tufanye hivi, kwa hiyo tunabadilika kutokana na mawazo ya watu,” amesema Gabo.
Katika hatua nyingine Gabo amemuelezea muigizaji Wema Sepetu ni mtu wa namna gani katika ufanyaji kazi hasa pale walipokuwa wakishoot filamu yake mpya ‘Kisogo’.
“Ni dada mmoja ambaye yupo na utaratibu wake, ukiufuata na kuusikiliza utafanya nae kazi vizuri sana na atakuwa yupo poa sana. Ukiwa nje ya huo utaratibu unaweza kumuona ni msumbufu na ukamuona kero kwenye kazi,” ameeleza Gabo.
“Sio kweli industry ipo vile vile, kwani jamaa alikuwa analeta changamoto kwa wacheza sinema wengi sana hivyo baada ya kuondoka ule ushindani ukawa umeshuka, hicho ndio kitu ambacho wanakikosa,” Gabo ameiambia Bongo Dot Home ya Times FM na kuongeza kuwa
“Lakini mimi nisema waendelee kuwa na mapenzi ya dhati ila wasisite kutoa malalamiko yao na kukosoa pale ambapo wanahisi pameenda tofauti kwa sababu changamoto za watu pekee ndio zinabadilisha.Tunajua hapo tunakosea inabidi tufanye hivi, kwa hiyo tunabadilika kutokana na mawazo ya watu,” amesema Gabo.
Katika hatua nyingine Gabo amemuelezea muigizaji Wema Sepetu ni mtu wa namna gani katika ufanyaji kazi hasa pale walipokuwa wakishoot filamu yake mpya ‘Kisogo’.
“Ni dada mmoja ambaye yupo na utaratibu wake, ukiufuata na kuusikiliza utafanya nae kazi vizuri sana na atakuwa yupo poa sana. Ukiwa nje ya huo utaratibu unaweza kumuona ni msumbufu na ukamuona kero kwenye kazi,” ameeleza Gabo.
Thursday, June 22, 2017

Trump: Ukuta wa Mexico utakuwa na nishati ya jua
Rais wa Marekani Donald Trump
amewaambia wafuasi wake kwamba pendekezo lake la ukuta katika mpaka na
Mexico litakuwa na paneli za kunasa miale ya jua.
Akihutubia
mkutano wa hadhara katika jimbo la Iowa, alisema kuwa paneli hizo za jua
zitatoa kawi na kusaidia kulipia ujenzi wa ukuta huo wenye utata.Alisema kuwa pendekezo hilo ni lake: Ni pendekezo zuri sio, hatahivyo paneli za jua zimeshirikishwa katika muundo wa ukuta huo uliowasilishwa na baadhi ya kampuni.
Wakati wa kampeni yake, bwana Trump aliahidi kujenga ukuta katika mpaka na Mexico ili kuzuia wahamiiaji haramu na ulanguzi wa dawa za kulevya.
Amesisitiza kuwa atailazimisha Mexico kulipia ujenzi huo , lakini rais wa taifa hilo Enrique Pena Nieto amepinga mpango huo.
Bwana Trump aliuambia umati uliomshangilia katika mkutano wa kampeni kwamba atatoa pendekezo ambalo hakuna mtu amewahi kulisikia.
''Tunafikiria kitu ambacho ni cha kipekee ,tunazungumzia kuhusu mpaka wa kusini, kuna jua jingi, na joto jingi pia''.
''Tunafikiria kujenga ukuta wa viage vya jua ambao utatengeza kawi na kujilipia. Njia hii Mexico italazimika kulipa fedha kidogo na hilo ni wazo zuri sio?''

Barakah The Prince: Sitaki kumpa mtu ‘kiki’
Barakah The Price ameamua kujibu mapigo baada ya Bright kuongea kuwa
hajui kuandika mistari na amekuwa akirudia rudia maneno katika nyimbo
zake
Akiongea kwenye E News ya EATV, Barakah amesema hawezi kuongelea lolote kuhusiana na hilo kwa kuwa hataki kuendelea kumpa kiki msanii mwenzake huyo ambaye alimshirikisha kwenye wimbo wa ‘Nitunzie’.
“Hiyo inaitwa unatafuta kiki kwa pikipiki, mimi siwezi kuongea nitakuwa nachafua brand yangu ya Rock Star na unajua mimi nikiongea watu wanazingatia sana, hivyo siwezi kuongelea watu kama hao katika interview zangu,” amesema msanii huyo.
Barakah ameongeza kwa kudai kuwa hamfahamu msanii anayeitwa Bright kwa kuwa anafanya kazi na wasanii wengi chipukizi.
Akiongea kwenye E News ya EATV, Barakah amesema hawezi kuongelea lolote kuhusiana na hilo kwa kuwa hataki kuendelea kumpa kiki msanii mwenzake huyo ambaye alimshirikisha kwenye wimbo wa ‘Nitunzie’.
“Hiyo inaitwa unatafuta kiki kwa pikipiki, mimi siwezi kuongea nitakuwa nachafua brand yangu ya Rock Star na unajua mimi nikiongea watu wanazingatia sana, hivyo siwezi kuongelea watu kama hao katika interview zangu,” amesema msanii huyo.
Barakah ameongeza kwa kudai kuwa hamfahamu msanii anayeitwa Bright kwa kuwa anafanya kazi na wasanii wengi chipukizi.

Stars kukwea pipa leo kwa ajili ya COSAFA
Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kinatarajia kukwea
pipa leo jioni kwenda Afrika Kusini kwaajili ya michuano ya COSAFA
inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Juni 25 mwaka huu.
Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kinatarajia kukwea pipa leo jioni kwenda Afrika Kusini kwaajili ya michuano ya COSAFA inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Juni 25 mwaka huu.
Tumefanya mazoezi kuanzia jumatatu mpaka leo asubuhi, mazoezi ambayo kiujumla naweza kusema tumekwenda vizuri, kwa sababu vijana walifika wote siku ya Jumapili usiku, Jumatatu tukaanza mazoezi mpaka leo asubuhi.
“Afya za wachezaji zipo vizuri, tulipata tatizo kidogo kwa Shabani ambaye yeye alipata matatizo kidogo akiwa mazoezini lakini wachezaji waliosalia wapo katika kiwango kizuri.
“Tunategema kwa mazoezi tuliyoyafanya leo jioni tutafanya safari ya kwenda Afrika Kusini vizuri kwaajili ya mashindano ya COSAFA na kule tutapata nafasi ya kufanya mazoezi siku kama mbili Ijumaa na Jumamosi na tarehe 25 tutacheza mchezo wetu wa kwanza katika mashindano hayo ambayo tumealikwa na tukifanya vizuri tutaendelea tukifanya vibaya tutarejea kwaajili ya CHAN inayotarajiwa kuchezwa Julai 15 mwaka huu” amesema kocha mkuu wa Taifa Stars, Salum Mayanga.
Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kinatarajia kukwea pipa leo jioni kwenda Afrika Kusini kwaajili ya michuano ya COSAFA inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Juni 25 mwaka huu.
Tumefanya mazoezi kuanzia jumatatu mpaka leo asubuhi, mazoezi ambayo kiujumla naweza kusema tumekwenda vizuri, kwa sababu vijana walifika wote siku ya Jumapili usiku, Jumatatu tukaanza mazoezi mpaka leo asubuhi.
“Afya za wachezaji zipo vizuri, tulipata tatizo kidogo kwa Shabani ambaye yeye alipata matatizo kidogo akiwa mazoezini lakini wachezaji waliosalia wapo katika kiwango kizuri.
“Tunategema kwa mazoezi tuliyoyafanya leo jioni tutafanya safari ya kwenda Afrika Kusini vizuri kwaajili ya mashindano ya COSAFA na kule tutapata nafasi ya kufanya mazoezi siku kama mbili Ijumaa na Jumamosi na tarehe 25 tutacheza mchezo wetu wa kwanza katika mashindano hayo ambayo tumealikwa na tukifanya vizuri tutaendelea tukifanya vibaya tutarejea kwaajili ya CHAN inayotarajiwa kuchezwa Julai 15 mwaka huu” amesema kocha mkuu wa Taifa Stars, Salum Mayanga.

Hata kama Ikulu hawajalipa bili ya maji, kata – Rais Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli
ameagiza taasisi zote hata ziwe za serikali zisipolipa bili za maji
zikatwe maji hata kama ni Ikulu.
Rais ameyasema hayo jana akiwa katika ziara yake ya siku tatu mkoani Pwani ambapo alizungumzia mradi wa maji na ulipaji katika taasisi zote.
“Mtu asipolipa bili, iwe taasisi yoyote hata kama ni Ikulu, narudia kusema kata.Kwa sababu tumezoa kudekezana, kwenye mawizara haya nafahamu, fedha za OC na hata fedha za bajeti wanazo, lakini suala la bili ya maji linakuwa si la lazima.”
Rais ameyasema hayo jana akiwa katika ziara yake ya siku tatu mkoani Pwani ambapo alizungumzia mradi wa maji na ulipaji katika taasisi zote.
“Mtu asipolipa bili, iwe taasisi yoyote hata kama ni Ikulu, narudia kusema kata.Kwa sababu tumezoa kudekezana, kwenye mawizara haya nafahamu, fedha za OC na hata fedha za bajeti wanazo, lakini suala la bili ya maji linakuwa si la lazima.”

Ujumbe wa Vanessa Mdee kwa Jux, atupa dongo gizani
Ni jambo zuri ukiona mtu wako wa karibu amefanikisha moja ya ndoto zake
katika maisha yake. Ni muhimu kumpatia ujumbe ambao utakaomtia moyo
katika kufanikisha mambo yake mengine aliyoyapangilia.
Vanessa Mdee ameamua kutumia vizuri fursa hiyo katika kumpongeza mpenzi wake Jux ambaye amehitimu masomo yake huko nchini China. Lakini katika ujumbe huo pia Vee amewapiga dongo watu waliokuwa wakimkejeli mwenza wake huyo kutokana na muimbaji huyo kutoonyesha picha yoyote akiwa na wanafunzi wenzake.
Kupitia mtandao wa Instagram, Vanessa ameandika:
Vanessa Mdee ameamua kutumia vizuri fursa hiyo katika kumpongeza mpenzi wake Jux ambaye amehitimu masomo yake huko nchini China. Lakini katika ujumbe huo pia Vee amewapiga dongo watu waliokuwa wakimkejeli mwenza wake huyo kutokana na muimbaji huyo kutoonyesha picha yoyote akiwa na wanafunzi wenzake.
Kupitia mtandao wa Instagram, Vanessa ameandika:
Congratulations @juma_jux U finally done and you done did it well. Hapo watu walikuwa wakiombaga picha za wewe darasani nadhani hii picha jibu la kutosha. Umeweza kufanya yote, MZIKI, BIASHARA NA SHULE… now that’s exceptional. Muda wa vibunda babaaa. Keep inspiring the YUTEEEEE
Sunday, June 18, 2017

Beyonce Knowles ajifungua pacha
Nyota wa muziki wa Pop nchini Marekani Beyonce amejifungua mapacha kulingana na vyombo vya habari nchini Marekani.
Vyombo
vya habari vya Entertainment Weekely, Us Weekly na People Magazine
vimethibitisha habari hizo lakini tarehe ya kuzaliwa na jinsia ya watoto
haijajulikana.Beyonce ambaye ni mkewe mwanamuziki wa mtindo wa Rap Jay Z alitangaza kwamba ni mjamzito katika picha ya Istangram mnamo mwezi Februari ambapo ni picha iliopendwa mno katika historia ya mtandao huo.
Hakujakuwa na tangazo rasmi kuhusu kujifungua huko kutoka kwa Beyonce na Jay Z mwenyewe.

Sitegemei kugombana na Alikiba - Baraka The Prince
Msanii Baraka The Prince amefunguka na kuweka wazi kuwa yeye hana
tofauti yoyote na Alikiba na kudai kuwa watu wa mitandaoni ndiyo
wamekuwa chanzo cha kusambaza maneno hayo kuonyesha yeye ana tofauti na
Alikiba.
Baraka The Prince amedai kuwa yeye hawezi kugombana na Alikiba na wala hategemei kuja kumkosea kwa kuwa ni moja kati ya watu ambao wanampenda sana yeye pamoja na sanaa yake.
Baraka The Prince amedai kuwa yeye hawezi kugombana na Alikiba na wala hategemei kuja kumkosea kwa kuwa ni moja kati ya watu ambao wanampenda sana yeye pamoja na sanaa yake.
Mbali na hilo Baraka The Prince amesema
kuwa mkali huyo wa Aje hivi sasa yupo kwenye maandalizi ya kuachia kazi
yake mpya baada ya Aje kusumbua zaidi ya mwaka mzima.
Alikiba na Baraka The Prince licha ya
kuwa chini la label moja ya RockStar4000 wasanii hao pia waliachia kazi
ya pamoja ambayo inafahamika kama 'Nisamehe' .

Mzee Yussuf afunguka kifo cha mkewe
Aliyekuwa mfalme wa taarab Alhaj Mzee Yussuf ambaye jana jioni
alimpoteza mke wake wa pili (Chiku) na kichanga wakati mkewe huyo
alipokuwa amepelekwa kujifungua katika Hospitali ya Amana, Ilala jijini
Dar es Salaam
Mzee Yussuf akiongea na mtangazaji Mwanne Othman kwenye kipindi cha Tam Tam za Mwambao, amesema kuwa miili ya vipenzi vyake hivyo itazikwa leo majira ya saa saba mchana Kisutu jijini Dar es Salaam na kusema msiba upo Kariakoo Mtaa wa Livingstone.
Mzee ameelezea kisa kizima jinsi ilivyokuwa mpaka mkewe na mtoto kupoteza maisha wakiwa hospitali, msikilize hapa


Mzee Yussuf akiongea na mtangazaji Mwanne Othman kwenye kipindi cha Tam Tam za Mwambao, amesema kuwa miili ya vipenzi vyake hivyo itazikwa leo majira ya saa saba mchana Kisutu jijini Dar es Salaam na kusema msiba upo Kariakoo Mtaa wa Livingstone.
Mzee ameelezea kisa kizima jinsi ilivyokuwa mpaka mkewe na mtoto kupoteza maisha wakiwa hospitali, msikilize hapa

Fifa yapendekeza dakika 60 mechi
Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) lina mpango wa kupunguza muda wa mchezo wa mpira wa miguu, kuwa dakika 30 kila kipindi
Bodi ya kimataifa ya soka duniani inatarajia kujadili pendekezo hilo
linalolenga kuondoa upotezaji muda kwa makusudi, tabia
inayofanywa wachezaji uwanjani.
Aidha waliopendekeza mpango huo wanasema kuwa mechi huchezwa kwa dakika 60 pekee kati ya 90 na muda uliosalia hutumiwa vibaya na wachezaji.
Pendekezo jingine ni wachezaji kutoruhusiwa kupiga mpira mara ya pili baada ya kipa kuupangua wakati wa penalti na iwapo penalti haikupigwa inavyostahili, mchezo utasitishwa na mpira wa adhabu kutolewa.
Mapendekezo mengine ni kama kuweka saa katika uwanja ambayo italingana na ile ya refa mbali pamoja na sheria mpya itakayoruhusu mchezaji kujipigia mpira au hata kutamba na mpira wakati anapopiga mpira wa adhabu
Aidha waliopendekeza mpango huo wanasema kuwa mechi huchezwa kwa dakika 60 pekee kati ya 90 na muda uliosalia hutumiwa vibaya na wachezaji.
Pendekezo jingine ni wachezaji kutoruhusiwa kupiga mpira mara ya pili baada ya kipa kuupangua wakati wa penalti na iwapo penalti haikupigwa inavyostahili, mchezo utasitishwa na mpira wa adhabu kutolewa.
Mapendekezo mengine ni kama kuweka saa katika uwanja ambayo italingana na ile ya refa mbali pamoja na sheria mpya itakayoruhusu mchezaji kujipigia mpira au hata kutamba na mpira wakati anapopiga mpira wa adhabu

Majeruhi wa Lucky Vicent kurejea nchini Agosti
Wanafunzi wa shule ya Lucky Vicent ya jijini Arusha,
walionusurika katika ajali iliyoua wanafunzi 32, walimu wawili na
dereva huenda wakarejea nchini baada ya miezi miwili.
Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu ametoa taarifa hiyo katika mtandao wake wa kijamii wa Instagram katika mahojiano na waandishi wa habari,akisema kuwa kuna matumaini ya watoto wote watatu kuweza kutembea na kuna uwezekano wa kurejea Tanzania baada ya miezi miwili ijayo.
Huku mtoto Doreen anatarajiwa kuhamishwa Madonna Center katika mji wa Lincoln, Jimbo la Nebraska kwa "Therapy" maalumu ya uti wa Mgongo wiki ijayo. Wanasema katika wote watatu Doreen ni muujiza mkubwa zaidi.
Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu ametoa taarifa hiyo katika mtandao wake wa kijamii wa Instagram katika mahojiano na waandishi wa habari,akisema kuwa kuna matumaini ya watoto wote watatu kuweza kutembea na kuna uwezekano wa kurejea Tanzania baada ya miezi miwili ijayo.
Huku mtoto Doreen anatarajiwa kuhamishwa Madonna Center katika mji wa Lincoln, Jimbo la Nebraska kwa "Therapy" maalumu ya uti wa Mgongo wiki ijayo. Wanasema katika wote watatu Doreen ni muujiza mkubwa zaidi.

Watu 25 wafariki dunia kwa moto Ureno
Watu 25 wamefariki dunia na wengine takriban 20 wamejeruhiwa kutokana na
moto mkubwa uliozuka katika msitu uliopo katikati mwa nchi ya Ureno.
Kwa mujibu wa taarifa ya awali iliyotolewa na serikali ya nchi hiyo imedai, watu wengi walifariki wakati walipokuwa wakijaribu kuyakimbia maeneo ya Pedrogao Grande yaliyopo Kusini Mashariki mwa mji wa Coimbra.
Naye waziri wa mambo ya ndani wa nchi hiyo, João Gomes amewaambia waandishi habari kuwa watu 16 wameteketea ndani ya magari yao hadi kufa, pale walipokabiliwa na moto huo mkubwa katika Wilaya ya Pedrógão Grande katika barabara inayounganisha miji ya Figueiro dos Vinhos na Castanheira de Pera.
Wakati huo huo waziri mkuu António LuÃs Santos da Costa, amesema hilo ni tukio baya zaidi kuwahi kutokea nchini humo katika miaka ya hivi karibuni.
Kwa mujibu wa taarifa ya awali iliyotolewa na serikali ya nchi hiyo imedai, watu wengi walifariki wakati walipokuwa wakijaribu kuyakimbia maeneo ya Pedrogao Grande yaliyopo Kusini Mashariki mwa mji wa Coimbra.
Naye waziri wa mambo ya ndani wa nchi hiyo, João Gomes amewaambia waandishi habari kuwa watu 16 wameteketea ndani ya magari yao hadi kufa, pale walipokabiliwa na moto huo mkubwa katika Wilaya ya Pedrógão Grande katika barabara inayounganisha miji ya Figueiro dos Vinhos na Castanheira de Pera.
Wakati huo huo waziri mkuu António LuÃs Santos da Costa, amesema hilo ni tukio baya zaidi kuwahi kutokea nchini humo katika miaka ya hivi karibuni.
Tuesday, June 13, 2017

Diamond asema Wema anamchango mkubwa sana kwenye Chibu Perfume
Msanii wa muziki Naseeb Abdul al-maarufu Diamond Platnumz ameamua kufunguka kwa kusema ukweli juu ya mchango wa aliyekuwa mpenzi wake Wema Sepetu kuhusiana na perfume yake ya "Chibu Perfume"
Huku Diamond akisema mara nyingi tu huwa anakutana na Wema sepetu tofauti na kushauriana juu ya mambo ya biashara
“Mimi na Wema labda watu hawajui sisi tunaongea sana wakati mwingine tunakutana tu sana lakini sio kwenye media. Tushakuwa kila mtu ana mahusiano yake tofauti yeye ana familia yake hata ukiangalia katika Perfume yangu lile neno THE SCENT YOU DESERVE alilitoa Wema” alisema Diamond.
Muimbaji huyo kwasasa yupo kwenye mahusiano ya Zari na tayari wamefanikiwa kupata watoto wawili.
Huku Diamond akisema mara nyingi tu huwa anakutana na Wema sepetu tofauti na kushauriana juu ya mambo ya biashara
“Mimi na Wema labda watu hawajui sisi tunaongea sana wakati mwingine tunakutana tu sana lakini sio kwenye media. Tushakuwa kila mtu ana mahusiano yake tofauti yeye ana familia yake hata ukiangalia katika Perfume yangu lile neno THE SCENT YOU DESERVE alilitoa Wema” alisema Diamond.
Muimbaji huyo kwasasa yupo kwenye mahusiano ya Zari na tayari wamefanikiwa kupata watoto wawili.

Taifa stars yajiandaa na COSAFA, kupiga kambi Afrika mashariki
Timu ya mpira wa miguu Taifa Stars yatarajiwa kuingia kambini hapo tarehe 14June kujiandaa na michuano
inayosimamiwa na Baraza la soka la Kusini mwa Africa liitwalo(COSAFA)
Michiano hiyo inatarajiwa kuanza June25 mwaka huu,huku Taifa stars ikitarajiwa kufika Afrika Kusini June20 pamoja na kocha wao Salum Mayanga akiwa na dhumuni la kufanya mabadiliko ya kufanya uteuzi mwingine kwa baadhi ya wachezaji na kutangaza majina ya wachezaji hao kesho ili wachezaji hao waweze kujiandaa ,na kuingia kambini ili wawe teyali
inayosimamiwa na Baraza la soka la Kusini mwa Africa liitwalo(COSAFA)
![]() |
Timu ya TaifaStars. |
Michiano hiyo inatarajiwa kuanza June25 mwaka huu,huku Taifa stars ikitarajiwa kufika Afrika Kusini June20 pamoja na kocha wao Salum Mayanga akiwa na dhumuni la kufanya mabadiliko ya kufanya uteuzi mwingine kwa baadhi ya wachezaji na kutangaza majina ya wachezaji hao kesho ili wachezaji hao waweze kujiandaa ,na kuingia kambini ili wawe teyali
Saturday, June 10, 2017

Mbaraka Yusuph kusaini mkataba mpya na Azam FC
Mara baada ya John Bocco
kuondoka ndani ya kikosi cha Azam FC, klabu hiyo imefanikiwa kunasa
saini ya straika mpya Mbaraka Yusuph aliyekuwa
Mbaraka Yusuph ni straika chipukizi aliyetamba msimu uliopita wa 2016/17 ndani ya kikosi cha Kagera Sugar katika Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara ambapo amesaini mkataba wa miaka miwili ndani ya klabu hiyo.
Ujio wa Mbaraka klabuni hapo utarejesha matumaini ya kuimarisha safu
ya ushambuliaji ambapo katika miaka ya hivi karibuni Azam FC iliwapoteza
mastraika waliokuwa na makali, Kipre Tchetche na John Bocco, hivyo
Mbaraka kwa kushirikiana na Waziri Jr aliyetua klabuni hapo hivi
karibuni akitokea Toto African ambayo imeshuka daraja wanatarajiwa
kutengeneza ushirikiano katika msimu ujao wa 2017/1akiitumikia klabu ya
Kagera Suga
Mbaraka Yusuph ni straika chipukizi aliyetamba msimu uliopita wa 2016/17 ndani ya kikosi cha Kagera Sugar katika Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara ambapo amesaini mkataba wa miaka miwili ndani ya klabu hiyo.
![]() |
Mbaraka akiweka saini ya kujiunga na Azam FC |

Darassa kunogesha SportPesa Super Cup
Darassa
ambaye ana ngoma nyingi zinazofanya vizuri ikiwemo 'Harasa Roho'
aliyoiachia siku za hivi karibuni, tayari amethibitisha kutumbuiza
katika fainali hiyo ambayo itawakutanisha "mashemeji derby" kutoka
Kenya.
"Jumapili hii ya tarehe 11, usikose pale
katika viwanja vya uhuru kwenye SportPesa Super Cup nitakuwepo pale
mapema kabisa kuanzia saa 6 mchana" alisema msanii huyo.
Fainali hiyo itakutanisha vilabu kutoka
nchini Kenya ambavyo ni Gor Mahia na Nakuru All Stars, baada ya klabu
zote nne za Tanzania kutolewa katika michuano hiyo.
Mshindi wa fainali hiyo atacheza mechi dhidi ya klabu kutoka Uingereza Everton.


Washauri wakuu wa waziri mkuu wa Uingereza wajiuzulu
Washauri wawili muhimu wa waziri mkuu wa Uingereza, Theresa May wamejiuzulu.
Pia
kuna ripoti kwamba wanachama wakuu wa chama tawala cha Uingereza, cha
Conservative, wametishia kuanza kutafuta kiongozi mpya, endapo washauri
hao hawatotolewa kazini.Mpambe wake, Nick Timothy, alisema anabeba dhamana kwa mchango wake katika kampeni ya chama, lakini alisema bado anaamini manifesto ilikuwa sawa, manifesto ambayo mwanachama mmoja maarufu alisema ni mbaya kabisa katika historia.
Msemaji wa chama amesema, mwenzake Bwana Timothy, Fiona Hill, piya amejiuzulu.
Bibi May anajaribu kuunda serikali ambayo haina wingi wa viti bungeni, kwa kutegemea chama kimoja cha Ireland Kaskazini.

Marekani yazitaka nchi za kiarabu kulegeza kamba kwa Qatar
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni
wa Marekani Rex Tillerson anasema kuwa nchi za Ghuba ni lazima zilegeze
hatua yao dhidi ya Qatar ambayo inalaumiwa na majirani zake kwa kuunga
mkono Ugaidi.
Saudi Arabia, Muungano wa nchi za kiarabu, Misri na
Bahrain walikata uhusiano wa usafiri na wa kidiplomasia na Qatar siku ya
Jumatatu.Bwana Tillerson anasema kuwa hatua hiyo inasabisha kuwepo madhara ya kibinadamu.
Licha la kumsifu Emir wa Qatar kwa kupuza uungwaji mkono makundi ya kigaidi, Bwana Tillerson anasema mengi yanahitaji kufanywa.
Naye Rais Trump ameishutumu Qatar kwa kufadhili ugaidi na kuitaka ikome.Awali Raisi Trump alikuwa ameadika kwenye mtandao wa Twitter akiunga mkono hatua ya kuitenga Qatar,na kudai kuwa alishiriki katika uamuzi uliochukuliwa na Saudi Arabia pamoja na nchi zingine.
Ndege za Qatar zilipigwa marufuku ya kutumia anga za baadhi ya majirani zake.Hatua hiyo ya ghafla
ilichukuliwa baada ya msukosuko ambao umedumu miaka kadha kati ya Qatar na majirani zake wa
Ghuba.

Mwana mitindo al-maalufu Amber Rose afutiwa picha yake ya utupu instagram
Mtandao wa kijamii wa Instagram wenye watumiaji zaidi ya milioni 500 duniani umefuta picha ya utupu ya mwanamitindo Amber Rose.
Picha hiyo ambayo Amber aliiweka kwenye mtandao huo, ilifutwa kutokana na kukosa maadili. Mara nyingi mtandao huo huziondoa picha ambazo zinaripotiwa kutokuwa na maadili.
Baada ya kufutwa picha hiyo ya utupu ambayo imewatoa udenda vidume wengi mitandaoni, Amber ameandika ujumbe mwingine kwenye mtandao huo unaoonyesha masikitiko yake baada ya kufutiwa picha hiyo huku mashabiki wakimuunga mkono kwa kitendo hicho.
Picha hiyo ambayo Amber aliiweka kwenye mtandao huo, ilifutwa kutokana na kukosa maadili. Mara nyingi mtandao huo huziondoa picha ambazo zinaripotiwa kutokuwa na maadili.
Baada ya kufutwa picha hiyo ya utupu ambayo imewatoa udenda vidume wengi mitandaoni, Amber ameandika ujumbe mwingine kwenye mtandao huo unaoonyesha masikitiko yake baada ya kufutiwa picha hiyo huku mashabiki wakimuunga mkono kwa kitendo hicho.

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais ataja Orodha ya watakaojiunga kidato cha tano
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi) George Simbachawene ametoa idadi
ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na
vyuo vya ufundi kwa mwaka 2017 huku jumla ya wanafunzi 2,999 wakiachwa.
Simbachawene ametoa kauli hiyo Ijumaa hii mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa ufaulu kwa mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 3.75 ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2015.
Waziri amedai kati ya wanafunzi 96,018 waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni wanafunzi 93,019 tu ndiyo waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi.
Waziri Simbachawene amesema kuwa jumla ya watahiniwa wote waliofanya mtihani wa kidato cha nne kwa shule kwa mwaka 2016 ni 349,524 huku waliofanya mtihani wa kujitegemea ni 47,751 ambapo watahiniwa waliofanya mtihani wa shule waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni 96,018 sawa na asilimia 27.60 ya watahiniwa waliofanya mtihani Tanzania Bara.
Simbachawene kuwa kutokana na mwongozo wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wa Mei 15, 2017 jumla ya wanafunzi 93,019 ndiyo wenye Sifa za kuchaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi kwa kuwa wamefaulu vigezo vyote vya msingi kama vilivyopangwa na Wizara ya elimu sayansi na teknolojia ambapo kati ya hao 92,998 ni wa shule na wanafunzi 21 ni wale waliosoma taasisi ya elimu ya watu wazima.
Aidha amewataka wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano kuwasili kwa wakati katika shule walizopangiwa July 17 mwaka huu na kwamba hakutakuwa na mabadiliko ya shule walizopangiwa.
“Na kama kuna mwanafunzi ambaye hataripoti kwenye shule aliyopangiwa kwa muda wa siku 14 nafasi yake itachukuliwa na mtu mwingine,” alisema Simbachawene.
Simbachawene ametoa kauli hiyo Ijumaa hii mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa ufaulu kwa mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 3.75 ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2015.
Waziri amedai kati ya wanafunzi 96,018 waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni wanafunzi 93,019 tu ndiyo waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi.
Waziri Simbachawene amesema kuwa jumla ya watahiniwa wote waliofanya mtihani wa kidato cha nne kwa shule kwa mwaka 2016 ni 349,524 huku waliofanya mtihani wa kujitegemea ni 47,751 ambapo watahiniwa waliofanya mtihani wa shule waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni 96,018 sawa na asilimia 27.60 ya watahiniwa waliofanya mtihani Tanzania Bara.
Simbachawene kuwa kutokana na mwongozo wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wa Mei 15, 2017 jumla ya wanafunzi 93,019 ndiyo wenye Sifa za kuchaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi kwa kuwa wamefaulu vigezo vyote vya msingi kama vilivyopangwa na Wizara ya elimu sayansi na teknolojia ambapo kati ya hao 92,998 ni wa shule na wanafunzi 21 ni wale waliosoma taasisi ya elimu ya watu wazima.
Aidha amewataka wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano kuwasili kwa wakati katika shule walizopangiwa July 17 mwaka huu na kwamba hakutakuwa na mabadiliko ya shule walizopangiwa.
“Na kama kuna mwanafunzi ambaye hataripoti kwenye shule aliyopangiwa kwa muda wa siku 14 nafasi yake itachukuliwa na mtu mwingine,” alisema Simbachawene.

Nicki Minaj amdiss tena Remy Ma
Mafahari hao wawili wamekuwa katika beef ya maneno tangu mwezi Disemba
mwaka jana, baada ya Remy kuanza kumchana Nicki katika wimbo wake wa
‘SHETHER’ lakini alijibiwa na mrembo huyo wa Young Money alijibu mapigo
kupitia nyimbo mbili alizoziachia mwezi Februari mwaka huu
Niki amedaiwa kurudi tena na kumchana Remy kwenye wimbo alioshiikishwa na 2 Chainz’s “Realize”, “I’ve been winning eight years consistently, at least respect it,” amerap mrembo huyo. “Papoose wrote that ‘Ether’ record, but I broke Aretha record / See this is chess, not checkers / You cannot check the checkers / Did Nas clear that ‘Ether’ record? / Nah, but I will complete the record.”
Mwezi Machi mwaka huu Remy alipohojiwa kwenye kipindi cha Another Round, alionekana kulimaliza bifu lake na Minaj huku akiwachana waliokuwa wakishangilia vita yao hiyo, je kwa kuchanwa tena kwenye wimbo huo ataendelea kubaki kimya au Nicki ndio kachkoza nyuki?
Niki amedaiwa kurudi tena na kumchana Remy kwenye wimbo alioshiikishwa na 2 Chainz’s “Realize”, “I’ve been winning eight years consistently, at least respect it,” amerap mrembo huyo. “Papoose wrote that ‘Ether’ record, but I broke Aretha record / See this is chess, not checkers / You cannot check the checkers / Did Nas clear that ‘Ether’ record? / Nah, but I will complete the record.”
Mwezi Machi mwaka huu Remy alipohojiwa kwenye kipindi cha Another Round, alionekana kulimaliza bifu lake na Minaj huku akiwachana waliokuwa wakishangilia vita yao hiyo, je kwa kuchanwa tena kwenye wimbo huo ataendelea kubaki kimya au Nicki ndio kachkoza nyuki?
Friday, June 9, 2017

Man United kumbwaga Ibrahimovic
Timu ya Man united huenda isimuongeze mkataba mpya mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic, mkataba wake wa sasa unamalizika Juni 30.
Zlatan mwenye miaka 35 alisaini mkataba wa mwaka mmoja na kukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi.Lakini mpaka sasa hakuna mjadala wa mkataba mpya na jeraha la goti alilopata mwezi April katika mchezo wa kombe la Europa ligi huenda likaongeza chachu ya kutopewa mkabata mpya.
Mshambuliaji huyu amecheza michezo 46 msimu huu na kufunga magoli jumla ya magoli 28.
![]() |
Zlatan Ibrahimovic |

Nini kitafanyika sasa baada ya uchaguzi Uingereza?
Nini hufanyika kukikosekana mshindi wa moja kwa moja katika uchaguzi mkuu?
Chama chenye wabunge wengi ndicho pekee huunda serikali?Si lazima. Chama chenye wabunge wengi baada ya kura zote kuhesabiwa maeneo yote 650, huwa kinatangazwa mshindi na kiongozi wake huwa waziri mkuu. Lakini hili huenda lisifanyike wakati huu kwa kuwa chama kilichoshinda hakina wingi wa wabunge. Inawezekana kwa chama kilichomaliza cha pili kuunda serikali.
Mtu hushinda vipi uchaguzi?
Njia rahisi zaidi kwa mtu kuwa waziri mkuu ni chama chake kupata wingi wa wabunge katika Bunge la Commons - kuwa na wabunge wengi kuliko wabunge wote wa vyama hivyo vingine wakijumlishwa.
Unahitaji wabunge wangapi kuwa na wingi?

Balozi wa China aipongeza bajeti ya Wizara ya Fedha
Barozi wa china hapa nchini mhe.Dkt. lu younqing ampongeza raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania
Mhe. Dkt. John Pombe magufuli na serikali yake kwa bajet yake nzuri iliyowasilishwa jana tarehe 8,june
mwaka huu hapo bungeni jijini dodoma na waziri wa fedha na mipango Dk. Phillip Mpango
Mhe. Dkt .Lu youqing ametoa pongezi hizo leo tarehe 9,june mwaka huu ikulu jijini dar es salaam muda mfupi tu baadi ya kufanya mazungumzo na Mhe. Raisi magufuli ambapo amesema kuwa bajeti iliyowasilishwa inamalengo ya kuongeza kasi ya maendeleo katika ujenzi wa miundombinu na ujenzi wa
viwanda.
Akiongeza kua kutokana na bajeti hiyo uchumi wa tanzania umeendelea kua imara na hivo umeweza kuwavutia wadau wengi wa maendeleo wakiwemo Benk ya Dunia (WB) na shirika la Fedha Duniani
(IMF) ambao wamekua wakishirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo yenye umuhimu mkubwa.
Mhe. Dkt. John Pombe magufuli na serikali yake kwa bajet yake nzuri iliyowasilishwa jana tarehe 8,june
mwaka huu hapo bungeni jijini dodoma na waziri wa fedha na mipango Dk. Phillip Mpango
Mhe. Dkt .Lu youqing ametoa pongezi hizo leo tarehe 9,june mwaka huu ikulu jijini dar es salaam muda mfupi tu baadi ya kufanya mazungumzo na Mhe. Raisi magufuli ambapo amesema kuwa bajeti iliyowasilishwa inamalengo ya kuongeza kasi ya maendeleo katika ujenzi wa miundombinu na ujenzi wa
viwanda.
Akiongeza kua kutokana na bajeti hiyo uchumi wa tanzania umeendelea kua imara na hivo umeweza kuwavutia wadau wengi wa maendeleo wakiwemo Benk ya Dunia (WB) na shirika la Fedha Duniani
(IMF) ambao wamekua wakishirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo yenye umuhimu mkubwa.

BEN POL:BARAKAH THE PRINCE ANA CHUKI NA MIMI
Baada ya Barakah The Prince kuuponda wimbo mpya wa Ben Pol ‘Tatu’ kwa
madai ni mbaya, Ben Pol amefunguka kwa kudai kuwa muimbaji huyo ambaye
anafanya vizuri na wimbo ‘Acha Niende’ ana chuki binafsi juu yake.
Ben amedai maoni ya Barakah The Prince yanaweza kuwa mazuri ya kuboresha na kujenga lakini anaona msuguano katika maoni hayo kutokana na mahusiano yao yalivyo hivi sasa .
“Hii source ya kutuchukia mimi na Jux ni kwasababu tulimpunguza kwenye umoja ambao tulikuwa tumeuanzisha wa kufanya show/tour hatukuwahi kusema hatukutaka kumuaibisha kwenye media na ilikuwa ni lazima tumpunguze kwasababu ya kukosa nidhamu,” alisema Ben Pol.
Aliongeza, “Mnapokuwa mnafanya kazi na mtu halafu mwengine ndio anakuwa Super Star halafu ni mdogo wenu, mnaenda kwenye Interview hatokei, mnahitaji kwenda kufanya sound check yeye kajifungia hotelini na msichana yani vitu hovyo hovyo yatupasa tumpunguze kwasababu inaonekana focus yake ipo chini
.Halafu ukimwambia haelewi. Kuanzia hapo ndio chuki ilipoanza sasa akitoa mawazo unaya-dout kidogo,huku ben pol akisema mimi napenda sana kupokea ushauri lakini inakuaje unapewa maoni na mtu ambae anakinyongo sasa hata mara ya mwisho nimemcheki unajua jibu lake ‘Shida yako nini’? ni message ya kawaida tu ya kishkaji halafu kesho unamsikia kwenye Radio eti anasema ‘mimi Ben Pol rafiki yangu sana nampenda sana’ ni unafki, lakini kwa yote mimi nampenda sana Barakah ni mdogo wangu”
Ben Pol, Barakah The Prince pamoja na Jux waliungana kwa pamoja na kufanya show ya pamoja iitwayo, LML ambayo ilifanyika kwa mara ya kwanza siku ya Valentine’s.
Pia katika mahojiano mbalimbali ambayo walikuwa walifanya walieleza kuwa shows za namna hiyo wangeendelea kuzifanya katika mikoa mbalimbali ya Tanzania.
Ben amedai maoni ya Barakah The Prince yanaweza kuwa mazuri ya kuboresha na kujenga lakini anaona msuguano katika maoni hayo kutokana na mahusiano yao yalivyo hivi sasa .
“Hii source ya kutuchukia mimi na Jux ni kwasababu tulimpunguza kwenye umoja ambao tulikuwa tumeuanzisha wa kufanya show/tour hatukuwahi kusema hatukutaka kumuaibisha kwenye media na ilikuwa ni lazima tumpunguze kwasababu ya kukosa nidhamu,” alisema Ben Pol.
Aliongeza, “Mnapokuwa mnafanya kazi na mtu halafu mwengine ndio anakuwa Super Star halafu ni mdogo wenu, mnaenda kwenye Interview hatokei, mnahitaji kwenda kufanya sound check yeye kajifungia hotelini na msichana yani vitu hovyo hovyo yatupasa tumpunguze kwasababu inaonekana focus yake ipo chini
.Halafu ukimwambia haelewi. Kuanzia hapo ndio chuki ilipoanza sasa akitoa mawazo unaya-dout kidogo,huku ben pol akisema mimi napenda sana kupokea ushauri lakini inakuaje unapewa maoni na mtu ambae anakinyongo sasa hata mara ya mwisho nimemcheki unajua jibu lake ‘Shida yako nini’? ni message ya kawaida tu ya kishkaji halafu kesho unamsikia kwenye Radio eti anasema ‘mimi Ben Pol rafiki yangu sana nampenda sana’ ni unafki, lakini kwa yote mimi nampenda sana Barakah ni mdogo wangu”
Ben Pol, Barakah The Prince pamoja na Jux waliungana kwa pamoja na kufanya show ya pamoja iitwayo, LML ambayo ilifanyika kwa mara ya kwanza siku ya Valentine’s.
Pia katika mahojiano mbalimbali ambayo walikuwa walifanya walieleza kuwa shows za namna hiyo wangeendelea kuzifanya katika mikoa mbalimbali ya Tanzania.
Thursday, June 8, 2017

STEVE NYERERE: MIMI SIJAIGIZA SAUTI ZA MBOWE NA WEMA.
Steve kakanusha kuhusika na uigizaji wa sauti za mtongozo zilizovuma baina ya watu wanaodaiwa kuwa ni Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na mrembo Wema Sepetu wa Bongo Movie..
“Kwanza mimi toka nimeanza kuigiza sauti sijawahi kuigiza sauti za viongozi wa chama fulani, Pili, kutongoza napo sio dhambi, ni sunna (akimaanisha ni jambo jema tu kwa mwanaume yoyote kulifanya).
Tatu, sio kila kitu ambacho kimefanywa na familia fulani basi Steve anahusika.
“Kwanza mimi toka nimeanza kuigiza sauti sijawahi kuigiza sauti za viongozi wa chama fulani, Pili, kutongoza napo sio dhambi, ni sunna (akimaanisha ni jambo jema tu kwa mwanaume yoyote kulifanya).
Tatu, sio kila kitu ambacho kimefanywa na familia fulani basi Steve anahusika.
![]() |
steve nyerere. |

Msanii Rayuu Afunguka Sababu za Kutokufunga Mwezi Mtukufu
MSANII kutoka Bongo Muvi, Alice Bagenzi ‘Rayuu’ amefunguka kuwa ugonjwa wa vidonda vya tumbo unaomsumbua umemfanya ashindwe kufunga kama alivyokuwa akifanya miaka ya nyuma.
Akizungumza na 3 Tamu, Rayuu amedai kuwa anaumia sana kutotimiza nguzo hiyo muhimu ya dini yake na anafanya kila awezalo kuhakikisha anautibu ugonjwa huo ili siku zijazo aweze kufunga.
“Nimekuwa nikijaribu kufunga lakini kabla siku haijaisha vizuri, vidonda vinatibuka hatari hivyo najikuta nikifungulia njiani, naumia sana kwa hali hii kwani napenda kufunga ila ndo hivyo sina jinsi,” alisema Rayuu
Akizungumza na 3 Tamu, Rayuu amedai kuwa anaumia sana kutotimiza nguzo hiyo muhimu ya dini yake na anafanya kila awezalo kuhakikisha anautibu ugonjwa huo ili siku zijazo aweze kufunga.
“Nimekuwa nikijaribu kufunga lakini kabla siku haijaisha vizuri, vidonda vinatibuka hatari hivyo najikuta nikifungulia njiani, naumia sana kwa hali hii kwani napenda kufunga ila ndo hivyo sina jinsi,” alisema Rayuu
Subscribe to:
Posts (Atom)