Saturday, June 10, 2017

Mbaraka Yusuph kusaini mkataba mpya na Azam FC


Mara baada ya John Bocco kuondoka ndani ya kikosi cha Azam FC, klabu hiyo imefanikiwa kunasa saini ya straika mpya Mbaraka Yusuph aliyekuwa
Mbaraka Yusuph ni straika chipukizi aliyetamba msimu uliopita wa 2016/17 ndani ya kikosi cha Kagera Sugar katika Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara ambapo amesaini mkataba wa miaka miwili ndani ya klabu hiyo.
Mbaraka akiweka saini ya kujiunga na Azam FC
Ujio wa Mbaraka klabuni hapo utarejesha matumaini ya kuimarisha safu ya ushambuliaji ambapo katika miaka ya hivi karibuni Azam FC iliwapoteza mastraika waliokuwa na makali, Kipre Tchetche na John Bocco, hivyo Mbaraka kwa kushirikiana na Waziri Jr aliyetua klabuni hapo hivi karibuni akitokea Toto African ambayo imeshuka daraja wanatarajiwa kutengeneza ushirikiano katika msimu ujao wa 2017/1akiitumikia klabu ya Kagera Suga

    Choose :
  • OR
  • To comment
No comments:
Write comments