Beki wa Yanga Hassan Kessy amesema ujio wa mshambuliaji raia wa Uganda wa Klabu ya Simba Emmanuel Okwi haumtishi.
Kessy amesema siku zote anapenda akabane na mchezaji tegemeo wa timu
pinzani kwa ajili ya kumpa ushindani ili aone upungufu wake ili aweze
kuufanyia kazi.
"Naheshimu uwezo alionao Okwi lakini siyo kumuogopa
na katika kuthibitisha hilo, nitaanza kumuonyesha tutakapokutana kwenye
mechi ya Ngao ya Jamii," .
"Mimi na Okwi tunajuana kutokana na kuwahi
kukutana katika mechi mbalimbali mimi nikiwa nachezea Mtibwa Sugar na
yeye akicheza Simba, " amesema.
Kessy amesema anaamini ushindani
utakuwa wa hali ya juu kutokana na kila klabu kusajili kutokana na
mapungufu yaliyotokea katika msimu uliopita lakini yeye kwa upande wake
anaendelea kujipanga ili kuhakikisha anafanya vizuri katika msimu ujao.
Saturday, July 1, 2017
Sina hofu na ujio wa Okwi - Kessy
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Write comments