Darassa
ambaye ana ngoma nyingi zinazofanya vizuri ikiwemo 'Harasa Roho'
aliyoiachia siku za hivi karibuni, tayari amethibitisha kutumbuiza
katika fainali hiyo ambayo itawakutanisha "mashemeji derby" kutoka
Kenya.
"Jumapili hii ya tarehe 11, usikose pale
katika viwanja vya uhuru kwenye SportPesa Super Cup nitakuwepo pale
mapema kabisa kuanzia saa 6 mchana" alisema msanii huyo.
Fainali hiyo itakutanisha vilabu kutoka
nchini Kenya ambavyo ni Gor Mahia na Nakuru All Stars, baada ya klabu
zote nne za Tanzania kutolewa katika michuano hiyo.
Mshindi wa fainali hiyo atacheza mechi dhidi ya klabu kutoka Uingereza Everton.

No comments:
Write comments