Mlinda mlango wa Azam FC na timu ya taifa ya Tanzania Aishi Salum
Manula, amekanusha kusaini na Klabu ya Simba huku akiongeza kuwa vipo
vilabu vingi vya hapa nchini alivyofanya navyo mazungumzo na muda
ukifika itajulikana na timu gani ataitumikia.
Aishi amekiri kuwa sasa yeye bado ni mlinda mlango wa Azam FC lakini ameshafanya nao mazungumzo na wamekubaliana kuondoka pale tu mkataba wake utakapoisha, huku akiongeza ya kuwa amepata ofa nyingi za vilabu vya ndani lakini kwa sasa bado sio muda mwafaka wa kutaja klabu atakayojiunga nayo baada ya kumalizana na Azam FC.
“Cha kusema kuhusiana na
suala la mimi kutoka Azam FC ilo niwahakikishie mashabiki na wapenda
Soka Watanzania kwamba ni kweli mkataba wangu utakapoisha Azam FC
nitaondoka ndani ya Azam lakini kuhusiana na ofa ni kweli kuna ofa
nyingi nimepata ndani ya nchi na tuliweza kuzungumza na hizo klabu
ambazo zinanihitaji na mazungumzo yameenda vizuri na yanaendelea vizuri
kwa ujumla” amesema Aishi Manula.
“Mimi sijasaini Simba na
nasikia kuna mkataba unaonyesha kwamba nimesaini Simba, hizo nadhani ni
watu wanajitahidi kutaka kujua au kuwathibitishia mashabiki waamini
kwamba nimesaini Simba lakini sio kweli, na kama ningekuwa nimesaini
Simba nadhani wao wenyewe wangeshanitangaza, ” amesema Aishi Manula.
“Kuhusiana na kujiunga na klabu yoyote hapa nchini bado na sio muda mwafaka wa mimi kutaja Klabu ambayo nitaenda kujiunga nayo lakini wakae tayari wakinisubiri mkataba wangu utakapoisha Julai mwaka huu ndani ya Azam FC nitaweka wazi wapi naenda lakini kuhusiana na mkataba sio kweli na sijasaini na timu yoyote” amesema Aishi Manula
No comments:
Write comments