Waziri wa Mambo ya ndani na Mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi Mkoani
Singida, Mwigulu Nchemba amefunguka na kuwataka watu wanaotaka haki za
ushoga watafute nchi ya kwenda ambayo isatoa haki hiyo lakini si
Tanzania.
Mwigulu Nchemba anasema kama kuna taasisi yoyote imesajilikuwa nchini na inafanya kampeni za haki za ushoga basi atazifutia usajili huo na watu wake kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
"Wanaotaka haki za ushoga
watafute tu nchi yao nyingine ambayo inaruhusu mambo hayo wakakae huko,
kama ni taasisi imesajiliwa kwenye nchi yetu tukaigundua inafanya
kampeni ya haki hizo na bahati nzuri zinasajiliwa Wizara ya Mambo ya
Ndani nitazifutia usajili wao, na kama ni raia wa Tanzania anaendesha
kampeni hizo tutamkamata na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria, na kama
si raia amekuja kwenye nchi yetu kuja kuendesha haki hizo tutampa amri
ya kuondoka ndani ya nchi yetu hatapata fursa hata ya kuchomoa chaji ya
simu kwenye soketi ya umeme" alisisitiza Mwigulu Nchemba .
No comments:
Write comments