Sunday, June 18, 2017

Beyonce Knowles ajifungua pacha

Nyota wa muziki wa Pop nchini Marekani Beyonce amejifungua mapacha kulingana na vyombo vya habari nchini Marekani.
Vyombo vya habari vya Entertainment Weekely, Us Weekly na People Magazine vimethibitisha habari hizo lakini tarehe ya kuzaliwa na jinsia ya watoto haijajulikana.

 Beyonce ambaye ni mkewe mwanamuziki wa mtindo wa Rap Jay Z alitangaza kwamba ni mjamzito katika picha ya Istangram mnamo mwezi Februari ambapo ni picha iliopendwa mno katika historia ya mtandao huo.
Wawili hao tayari wana mwana wa kike, kwa jina Blue Ivy aliye na umri wa miaka mitano.
Hakujakuwa na tangazo rasmi kuhusu kujifungua huko kutoka kwa Beyonce na Jay Z mwenyewe.

    Choose :
  • OR
  • To comment
No comments:
Write comments