Friday, July 21, 2017

Waziri Mkuu ampa miezi miwili Mkurugenzi wa Halmashauri Songwe

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ampa miezi miwili kuanzia leo Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Songwe, Elias Nawera abadili mwenendo wake kiutendaji na ashirikiane vizuri na Mkuu wa wilaya hiyo Samwel Jeremiah

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo Alhamisi hii, wakati akizungumza na watumishi wa wilaya ya Songwe akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Songwe.
Amesema watumishi wote wanatakiwa kufanya kazi kwa ushirikiano ili malengo ya Serikali ya kuwahudumia wananchi yaweze kufikiwa. Pia waheshimiane sehemu za kazi na kila mtu azingatie mipaka ya madaraka yake.
“Mkurugenzi hapa hamsikilizi Mkuu wa wilaya anaondoka kituo cha kazi bila ya kuaga na amewagawa wakuu wa Idara. Namtaka afanye mabadiliko ya utendaji wake ndani ya miezi miwili na Mkuu wa Mkoa fuatilia jambo hili,” alisisitiza Waziri Majaliwa.
Pia amewaagiza Wakuu wa Wilaya wote wasimamie utendaji wa wakurugenzi wa Halmashauri kwenye maeneo yao ili kuhakikisha wananchi wanahudumiwa ipasavyo.”Serikali hii si ya mchezo. Serikali hii inahitaji watumishi waadilifu wa kuwatumikia Watanzania.”
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Bibi Chiku Galawa amesema wamejipanga kuhakikisha changamoto zote zinazoukabili mkoa zinaboreshwa pamoja na kufikia malengo ifikapo 2020

Man United waichakaza Man City bila huruma

Klabu ya soka ya Manchester United imeendeleza ushindi katika mechi zake za kirafiki huko nchini Marekani

United ambao walikuwa wakicheza na majirani zao Manchester City asubuhi hii katika mechi ya kirafiki ya kombe la International Champions Cup 2017 mjini Houston, imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.
Magoli hayo ya Man United yaliyofungwa  na Romelu Lukaku dakika ya 37 na Marcus Rashford dakika ya 39.


Picha: Diamond na mama yake walivyowasili kwenye msiba wa mama yake Zari

Msanii Diamond Platnumz pamoja na mama yake mzazi Bi Sandra wamefanikiwa kuhudhuria katika msiba wa mama yake Zari The Bosslady nchini Uganda.

 Bosi huyo wa WCB amewasili jana katika msiba huo ambao kwa mujibu wa taarifa aliyoitoa Zari kupitia mtandao wa Instagram, marehemu alifariki asubuhi ya siku ya jana (Alhamisi). Babu Tale naye ameambatana na Diamond katika msiba huo.

Harmorapa azidi kumganda Amber Lulu

Licha ya ukaribu wao kuchukuliwa kama kiki, msanii Harmorapa amezidi kusisitiza yupo katika mahusiano ya kimapenzi na video vixen Amber Lulu licha ya mrembo huyo kuwahi kukanusha hilo

Harmorapa ambaye amekuwa akivutia watu wengi kwa vituko vyake, ameiambia Boys Boys ya TV1 kuwa yeye kama kijana wa kiume ni lazima awepo katika mahusiano.

“Unajua siku zote kama ni mwanaume, halafu mwanaume rijali ni lazima uwe kwenye mahusiano ya kimapenzi, kwa hiyo mimi nina mpenzi, kuoa bado hata mtoto sina. Kwa sasa ni mtu famous, nilishamtaja ili kuna wengine hawamfahamu ni Amber Lulu,” amesema Harmorapa.

Saturday, July 1, 2017

Jacob Zuma na makamu wake walazimishwa kusalimiana


Aliyekuwa mke wa rias wa kwanza wa Afrika Kusini Nelson Mandela,
Winnie Madikizela Mandela aliwalazimisha viongozi wawili maaruf nchini humo rais Jacob Zuma na makamu wa rais Cyril Ramaphosa kusalimiana.
Wawili hao walikuwa katika mkutano wa chama cha ANC mjini Johannesburg.
Bwana Ramaphosa anataka kumrithi rais Zuma na amekuwa akimkashifu rais huyo kwa uhusiano wake na familia ya Gupta.


Mojawapo ya mambo yaliyobainika katika barua pepe zilizotajwa kuwa 'Guptaleaks', ni kwamba rais Zuma alikuwa amepanga kwenda kuishi katika miliki za Kiarabu UAE.
Madai ambayo yamekanwa.
Mengine yalionyesha kuwa familia hiyo ya Gupta imekuwa na ushawishi mkubwa serikalini.

Trump: Tumechoka kuivumilia Korea Kaskazini

Rais wa Marekani Donald Trump anasema muda wa uvumilivu wa kimikakati kwa Korea Kaskazini umekamilika sasa.
Katika hotuba ya pamoja na rais wa Korea Kusini Moon Jae, kwenye ikulu ya White house, Trump amesema kwamba vitisho vya Korea Kaskazini vinafaa kupata majibu ya kijasiri.
Hata hivyo, Trump amesema ni muhimu kuwe na ushirikiano katika kugawana mzigo wa kuhakikisha
usalama.
Rais wa Korea Kusini amesema kwamba taifa lake litaweka marekebisho ya kiuslama na kujenga msingi dhabiti wa kujikinga.
Rais Moon pia amesema ni muhimu kuendelea na majadiliano na viongozi wa Korea Kaskazini.

Kwengineko, Bwana Moon alisema kuwa ni muhimu kuendelea kujadiliana na viongozi wa Korea Kaskazini.
Bwana Moon alisema kuwa swala la Korea Kaskazini linafaa kupewa kipaumbele wakati wa mazungumzo akisisitiza kuwa ni usalama thabiti pekee unaoweza kuleta amani katika eneo zima la Pacific.

Akizungumza katika Ikulu ya Whitehouse, bwana Trump alisema kuwa wakati wa kuvumiliana na utawala Korea Kaskazini umefeli miaka mingi akiongezea: Kwa kweli uvumilivu huo umekwisha
 Kiongozi huyo wa Marekani amesema kuwa serikali yake sasa inafanya kazi na Korea Kusini pamoja na Japan wakiwemo washirika wengine duniani kuchukua hatua kadhaa za kidiplomasia, usalama na kiuchumi ili kuwalinda washirika wake pamoja na raia wa Marekani dhidi ya janga hilo kwa jina Korea Kaskazini.

Lionel Messi alivyouaga ukapera!

Nyota wa timu ya Barcelona, Lionel Messi amefunga ndoa ya kifahari na mpenzi wake wa utotoni Antonella Roccuzzo ambaye pia ni mzazi mwenzake wa watoto wawili.

Ndoa hiyo imefungwa huko Rosario City nchini Argentina usiku wa kuamkia leo huku ikuhudhuriwa na mastaa kibao wa soka kama kina Xavi, Carles Puyol, Cesc Fabregas, Samuel Eto'o, Luis Suarez, Jordi Alba na Sergio Busquets.
Wanasoka wengine walioudhuria harusi hiyo ni  Sergio Agüero, Ezequel Lavezzi, Javier Mascherano na Angel Di Maria.

Sina hofu na ujio wa Okwi - Kessy

Beki wa Yanga Hassan Kessy amesema ujio wa mshambuliaji raia wa Uganda wa Klabu ya Simba Emmanuel Okwi haumtishi.

 Kessy amesema siku zote anapenda akabane na mchezaji tegemeo wa timu pinzani kwa ajili ya kumpa ushindani ili aone upungufu wake ili aweze kuufanyia kazi.
"Naheshimu uwezo alionao Okwi lakini siyo kumuogopa na katika kuthibitisha hilo, nitaanza kumuonyesha tutakapokutana kwenye mechi ya Ngao ya Jamii," .
"Mimi na Okwi tunajuana kutokana na kuwahi kukutana katika mechi mbalimbali mimi nikiwa nachezea Mtibwa Sugar na yeye akicheza Simba, " amesema.
Kessy amesema anaamini ushindani utakuwa wa hali ya juu kutokana na kila klabu kusajili kutokana na mapungufu yaliyotokea katika msimu uliopita lakini yeye kwa upande wake anaendelea kujipanga ili kuhakikisha anafanya vizuri katika msimu ujao.

Spika Ndugai awaonya wabunge wanaochafua hali ya hewa bungeni

Spika wa Bunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai amewaonya wabunge wanaochafua hali ya hewa kwa kauli za matusi na maudhi bungeni waache mara moja kwani  vitendo
 hivyo ni vibaya kwa wapiga kura wao huku akiwashangaa kuwa huenda wakawa na matatizo yao binafsi yanayowasumbua.
Mhe. Ndugai amesema hayo jana mjini Dodoma baada ya kuwepo kwa baadhi ya wabunge wanaotoa kauli zisizokuwa rasmi katika vikao vya bunge bila kufikiria kwamba wanachokifanya hakina taswira nzuri kwa wapiga kura wao pamoja na Bunge.
Huku Ndugai akisema kuwa
“Unajua sisi tunaokaa hapa mezani hatuchangii kama nyinyi, kazi yetu ni kuwapa nafasi  mseme, wakati mwingine zinatoka shutuma ambazo hatuna nafasi ya kubishana au kulumbana lakini wakati mwingine ni vizuri kutumia fursa hizi kusafisha baadhi ya mambo. Binadamu ni lazima uwe na staha ile ndogo tu kuwaheshimu binadamu wenzako,”  akiwa amesisitiza kuwa
“Katika bunge letu kinacholeta matatizo humu ndani ni tabia na lugha, tukirekebisha hayo mawili tutaenda vizuri tu lakini najua kundi hili ni kubwa hatuwezi kuwa wote tupo sawa, nitaendelea kulisemea lakini pale kwenye ulazima tutachukua hatua,”

Hata hivyo Mh Ndugai amewaonya wabunge wanaochafua hali ya hewa bungeni kwa lugha chafu waache vitendo hivyo kwani hao ndiyo wanaoudhi kwa kauli zao za kusema bunge ni dhaifa huku akisisitiza kuwa wabunge aliowapa adhabu bado adhabu yao iko pale pale ya kukaa nje ya bunge kwa mwaka mmoja.


TCRA yazitaka kampuni za simu kusitisha matangazo kwenye miito ya simu

Mamlaka ya Mawasiliano nchini Tanzania (TCRA), imewataka wamiliki wa mitandao ya simu nchini kusitisha matangazo yanayosikika kabla ya muito wa simu pindi mteja anapopiga simu


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA,James Kilaba ambapo amesema kuwa matangazo hayo yamekuwa kero kwa watumiaji wa mitandao ya simu nchini.

Aidha Kilaba anazitaka kampuni za simu kusitisha matangazo pindi mtu anapopiga simu kabla ya muito huku akisema matangazo hayo yamekuwa kero kwa watumiaji wa mitandao ya simu na hivyo kutoa wito kwa kampuni za simu zote kurudi katika utaratibu wa kawaida mtu anapopiga simu akutane na miito ya kawaida na si matangazo.
“Tunachoongelea ni kwamba kama mtu unapiga simu moja kwa moja ianze ringtone au yenyewe imeweka au mwenyewe umechagua lakini tunataka ianze kwenye ringtone ianze kuring kama hapatikani iseme ni busy tone moja kwa moja sio kwamba uanze utangulizi ukiisha huo ndio ije ringtone sasa hivi ndicho kinachotokea kwa baadhi ya makampuni ya simu,” alisema Kilaba.

Adele akatisha tamasha lake ghafla

Msanii wa muziki kutoka nchini Uingereza Adele, amelazimika kukatisha tamasha lake la 123-date world tour kwa kile kinachodaiwa kupata madhara katika koo lake(vocal cords).


Muimbaji huyo mwenye mashabiki lukuki amelazimika kukatisha show zake mbili zijazo baada ya show yake ya Juni 29 aliyofanya uwanja wa Wembley nchini humo. Kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram jana aliamua kuwaandikia mashabiki zake waliokuwa wakiisubiria tamasha hilo kuwa atashindwa kuendelea na tamasha kutokana na maradhi aliyonayo.

Jay Z amtumbua mama yake

Albamu ya 13, ya rapper Jay Z imetoka na mojawapo ya ngoma inayopatikana katika albamu hiyo ya 4:44 imeeleza kuwa mama yake ni mtu anayeshiriki mapenzi ya jinsia moja.


Ngoma hiyo inayoitwa ‘Smile’ aliyomshirikisha mama yake imeweza kuthibitisha kuwa mama mzazi wa rapper huyo(Gloria Carter) kuwa ni mtu anayeshiriki mapenzi ya jinsia moja, Katika ngoma hiyo inasema kuwa “Mama had four kids, but she’s a lesbian,” he raps on the No I.D.-produced track. “Had to pretend so long, that she’s a thespian / Had to hide in the closet, so she medicate / Society’s shame and the pain was too much to take / Cried tears of joy when you fell in love / Don’t matter to me if it’s a him or her.”

Pia katika outro ya ngoma hiyo mama yake Jay amesikika akiimba kwa kusema “Living in the shadow/ Can you imagine what kind of life it is to live? In the shadows people see you as happy and free, because that’s what you want them to see. Living two lives, happy, but not free.”
Mama akazidi kutiririka “Living in the shadow feels like the safe place to be/ No harm for them, no harm for me. But life is short, and it’s time to be free. Love who you love, because life isn’t guaranteed. Smile.”
Hiyo ni baadhi ya mistari inayopatikana katika ngoma hiyo ili uweze kusikiliza kwa urefu zaidi cha msingi ni kuhakikisha unanunua albamu hiyo kupitia mtandao wa Tidal.

Monday, June 26, 2017

Aishi:Sijasaini mkataba Simba

Mlinda mlango wa Azam FC na timu ya taifa ya Tanzania Aishi Salum Manula, amekanusha kusaini na Klabu ya Simba huku akiongeza kuwa vipo vilabu vingi vya hapa nchini alivyofanya navyo mazungumzo na muda ukifika itajulikana na timu gani ataitumikia.

Aishi amekiri kuwa sasa yeye bado ni mlinda mlango wa Azam FC lakini ameshafanya nao mazungumzo na wamekubaliana kuondoka pale tu  mkataba wake utakapoisha, huku akiongeza ya kuwa amepata ofa nyingi za vilabu vya ndani lakini kwa sasa bado sio muda mwafaka wa kutaja klabu atakayojiunga nayo baada ya kumalizana na Azam FC.
 “Cha kusema kuhusiana na suala la mimi kutoka Azam FC ilo niwahakikishie mashabiki na wapenda Soka Watanzania kwamba ni kweli mkataba wangu utakapoisha Azam FC nitaondoka ndani ya Azam lakini kuhusiana na ofa ni kweli kuna ofa nyingi nimepata ndani ya nchi na tuliweza kuzungumza na hizo klabu ambazo zinanihitaji na mazungumzo yameenda vizuri na yanaendelea vizuri kwa ujumla” amesema Aishi Manula.

Aishi amekanusha yeye kusaini mkataba na klabu ya Simba
“Mimi sijasaini Simba na nasikia kuna mkataba unaonyesha kwamba nimesaini Simba, hizo nadhani ni watu wanajitahidi kutaka kujua au kuwathibitishia mashabiki waamini kwamba nimesaini Simba lakini sio kweli, na kama ningekuwa nimesaini Simba nadhani wao wenyewe wangeshanitangaza, ” amesema Aishi Manula.

Aishi amesisitiza kuwa mpaka sasa bado hajajiunga na klabu yoyote hapa nchini huku akiwataka mashabiki kuwa tayari kwani muda utakapofika ataweka wazi kila kitu.
“Kuhusiana na kujiunga na klabu yoyote hapa nchini bado na sio muda mwafaka wa mimi kutaja Klabu ambayo nitaenda kujiunga nayo lakini wakae tayari wakinisubiri mkataba wangu utakapoisha Julai mwaka huu ndani ya Azam FC nitaweka wazi wapi naenda lakini kuhusiana na mkataba sio kweli na sijasaini na timu yoyote” amesema Aishi Manula

Manowari ya Uingereza kuanza kufanyiwa majaribio leo

Manowari mpya ya Uingereza inatarajwa kuanza majaribio ya baharini leo.
HMS Queen Elizabeth ndiyo meli kubwa zaidi kuwai kuundwa kwa jeshi la wanamaji la Uingereza iliwa na uwanja wa ndege wenye ukubwa wa viwanja vitatu vya soka.
Meli hiyo ni kubwa hadi itahitaji kusubiri kushuka kwa viwango vya maji kuweza kupititia eneo la Forth bridges.


Manowari mpya ya Uingereza inatarajwa kuanza majaribio ya baharini leo.
HMS Queen Elizabeth ndiyo meli kubwa zaidi kuwai kuundwa kwa jeshi la wanamaji la Uingereza iliwa na uwanja wa ndege wenye ukubwa wa viwanja vitatu vya soka.
Meli hiyo ni kubwa hadi itahitaji kusubiri kushuka kwa viwango vya maji kuweza kupititia eneo la Forth bridges.

Uturuki yazuia maandamano ya wapenzi wa jinsia moja

Mamlaka nchini Uturuki imevunjilia mbali gwaride la wapenzi wa jinsia moja katika mji wa Istanbul, kwa mwaka wa tatu mfululizo.
Polisi walitumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya watu waliojaribu kushiriki gwaride hilo na kuwakamata baadhi yao.
 Mamlaka inasema imechukua hatua hiyo ili kuzima tishio la makundi yanayopinga serikali kutumia gwaride hilo kuzusha vurugu.

 Wanaharakati wa kutetea haki ya wapenzi hao wa jinsia moja wamepuuzilia mbali madai hayo na kuongezea kuwa serikali inatumia vigezo hivyo kama sababu ya kuminya uhuru wa watu hao.
Wanamshutumu Rais Recep Tayyip Erdogan anayegemea maadili ya kiislamu kwa kujaribu kuliendesha taifa kwa kutumia mtazamo wake binafsi juu ya masuala fulani katika jamii.

Trump akosa kuandaa chakula cha Eid White House

Rais wa Marekani Donald Trump, amevunja tamaduni ya karibu miaka ishirini kwa kukosa kuandaa chakula cha jioni kuadhimisha kukamilika kwa mwezi mtukufu wa Ramadan.
Hafla hiyo inayoandaliwa katika ikulu ya White House imekuwa ikifanyika kila mwaka kutoka kipindi cha Rais Bill Clinton.
Sherehe za Eid al-Fitr ndio mwisho wa mfungo wa Ramadan wakati waislamu hufunga
Awali Bwana Trump amelaumiwa kwa kutumia maneno makali dhidi ya waislamu ikiwemo kampeni ya kutaka uchunguzi kufanyiwa misikiti nchini Marekani.
Alisema katika taarifa: "Kwa niaba ya watu wa Marekani na Melania ninatuma heri njema kwa waislamu wakati wanaposherehekea Eid al-Fitr.

Chakula cha kwanza cha Eid kilichoandaliwa Ikulu ya White House kiliandaliwa na Rais Thomas Jefferson mwaka 1805 kwa ujumbe kutoka Tunisia.
Sherehe hizo zilifufuliwa tena na Hillary Clinton mwaka 1996 wakati akiwa mama wa kwanza wa taifa.
Hafla hiyo ilianza kufanywa kila mwaka tangu mwaka 1999 na kuhudhuriwa na viongozi wa kiislamu mashuhuri nchini Marekani.

Wachezaji bongo tusiogope kwenda nje - Maguli

Mshambuliaji wa kimataifa anayeitumikia klabu ya Dhofar SC ya nchini Oman, Elias Maguli amewataka vijana wa Kitanzania wanaotaka kuendeleza vipaji vyao, nje ya nchi kujaribu pale wanapopata nafasi na sio kukata tamaa.

Maguli amesema, vijana wengi wamekuwa wakipata nafasi za kwenda katika majaribio katika timu mbalimbali za nje ya nchi lakini wamekuwa wakikatishwa tamaa na baadhi ya watu wanaowazunguka .

"Kwanza wanapopata nafasi waende. Hawawezi kupata taarifa kwamba kuna ubaguzi katika hiyo nchi unayotakiwa kwenda kabla hujafika. Fika kwanza ndio ujue matatizo yaliyopo katika hiyo nchi, na mimi nina imani kuna wachezaji wengi wamepata nafasi lakini labda wao wanapenda kucheza hapa nchini,” amesema Elias Maguli.

Maguli ameongeza kwa kuvitaka vilabu vya soka hapa nchini kuwaruhusu wachezaji ili waweze kutumia nafasi wanazozipata nje ya nchi
“Kunawachezaji wengine wameshapata nafasi lakini vilabu vimekuwa tatizo, kwani vilabu mara nyingi huwa vinawakatalia wachezaji na hata kutaja dau kubwa na ukiangalia sisi wachezaji wa hapa Tanzania katika viwango bado tupo chini, hivyo tunapopata nafasi ni lazima kuzitumia ili kuweza kukuza zaidi vipaji vyetu, ” alisisitiza Maguli.
Maguli amewataka wachezaji kutokuogopa changamoto katika soka kwani changamoto wanazokutana nazo ndizo zinasaidia kuweza kuwakuza katika soka.
“Unajua Tanzania kukiwa na wachezaji wengi wa kimataifa ingekuwa ni faida kwani kila mchezaji anapoitwa katika timu ya Taifa tungefanya vizuri zaidi ya hapa kwani kila mchezaji anakuja na uwezo wake aliofundishwa kutoka katika klabu yake, na pia tunajifunza vitu vingi katika maisha ya Soka, na tusiogope changamoto kwani changamoto hata hapa nchini zipo na ndizo zinazotusaidia kukua kisoka. Sasa kwa nini tuogope kwenda nje, tunahitaji kuwa wengi wa kimataifa, ” amesema Maguli.

Mwigulu Nchemba:wanaotaka ushoga watafute nchi ya kwenda

Waziri wa Mambo ya ndani na Mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi Mkoani Singida, Mwigulu Nchemba amefunguka na kuwataka watu wanaotaka haki za ushoga watafute nchi ya kwenda ambayo isatoa haki hiyo lakini si Tanzania.


Mwigulu Nchemba anasema kama kuna taasisi yoyote imesajilikuwa nchini na inafanya kampeni za haki za ushoga basi atazifutia usajili huo na watu wake kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

"Wanaotaka haki za ushoga watafute tu nchi yao nyingine ambayo inaruhusu mambo hayo wakakae huko, kama ni taasisi imesajiliwa kwenye nchi yetu tukaigundua inafanya kampeni ya haki hizo na bahati nzuri zinasajiliwa Wizara ya Mambo ya Ndani nitazifutia usajili wao, na kama ni raia wa Tanzania anaendesha kampeni hizo tutamkamata na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria, na kama si raia amekuja kwenye nchi yetu kuja kuendesha haki hizo tutampa amri ya kuondoka ndani ya nchi yetu hatapata fursa hata ya kuchomoa chaji ya simu kwenye soketi ya umeme" alisisitiza Mwigulu Nchemba .

Mbali na hilo Mwigulu Nchemba alipigia msumali kauli ya Rais dhidi ya wanafunzi ambao watapata ujauzito wakiwa shuleni na kusema watu wanaopinga jambo hilo wasitumie nguvu kubwa kupinga bali wajenge shule zao wao watoe hiyo haki ya kusomesha wanafunzi wajawazito au wale ambao tayari wamejifungua na siyo kulazimisha serikali ya Magufuli kufanya hayo

Okwi atema cheche

Mshambuliaji wa zamani wa kikosi cha Simba Emmanuel Okwi ambaye jana amerejea rasmi katika kikosi hicho baada ya kusaini mkataba wa kuitumikia Simba amefunguka na kusema amekuja kupambana kuhakikisha kuwa Simba inapata ubingwa na kufanya vizuri.

Okwi anasema amefurahi sana kurudi katika timu yake hiyo ya zamani ikiwa chini ya viongozi wapya ambao ambao wanaonekana na njaa ya timu yao kufanya vizuri zaidi hivyo ameahidi kushirikiana nao na kuhakikisha timu hiyo inafanya vyema.

Marufuku kusafirisha chakula nje - Majaliwa

Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa apiga marufuku usafirishaji wa chakula nje ya nchi bila kibali na kuwataka wafanyabiashara kuuza chakula kwenye maeneo yenye uhaba nchini.


Mhe. Majaliwa ametoa agizo hilo leo, wakati akihutubia Baraza la Iddi katika msikiti wa Masjid Riyadh mjini Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo amesema kuwa kuna maeneo ambayo wananchi hawakupata chakula vizuri kutokana na uhaba wa mvua hivyo wafanyabiashara wapeleke chakula kwenye maeneo hayo.

Waziri Mkuu amesema Serikali bado haijatoa kibali cha kutoa chakula nje ya nchi na kama kuna umuhimu kwa anayetaka anatakiwa akaombe ambapo kibali hicho kitahusu , kusaga kwaajili ya kusafirisha unga na siyo mahindi.

Waziri Mkuu Majaliwa amesema kuwa Serikali imepokea barua za maombi ya kupeleka chakula nchi jirani, lakini bado haijatoa ruhusa na kuonya wale watakao kamatwa wakisafirisha mahindi nje ya nchi kinyume na utaratibu, mahindi hayo yatataifishwa na kupelekwa kwenye ghala la Taifa na magari yatapelekwa polisi

Saida Karoli afunguka juu ya Darassa na Ray C

Msanii mkongwe wa muziki wa asili, Saida Karoli amewamiminia sifa kibao wasanii wa Bongo Fleva, Ray C na Darassa.
Saida ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya Orugambo, amesema hit song ya Darassa ‘Muziki’ ni vigumu kuja kushuka na kuwataka wasanii wengine hasa wa hip hop kuchukulia hilo kama somo.
“Wimbo wa Darassa utaendelea kuhit, utaendelea kuwa shule kwa waimbaji wa hip hop.
Nitapenda watumie akili alizotumia Darassa, mimi naamini wimbo wa Darassa hauwezi kushuka hata siku moja na Watanzania wengi walikuwa hawapendi muziki wa hip hop lakini Darassa kuonyesha njia kwa sababu sasa hivi hadi kwenye harusi wanaimba acha maneno weka muziki, hadi Bungeni,” Saida ameiambia Clouds FM.
Kwa upande wa Ray C Saida amesema licha ya msanii huyo kupitia matatizo mengi bado uwezo wake upo pale pale na kuna baadhi wamejaribu kumuiga ila wameshindwa.
“Kwa kweli Ray C nampenda sana kutoka moyoni tangu zamani, sauti yake ni nzuri haina mpinzania, wasichana wengi wamejaribu kuiga kuimba kama yeye, wanapenda mvuto wake na muonekano wake lakini wameshindwa,” amesema Saida na kuongeza.
“Na ukiangalia Ray C amepitia matatizo makubwa sana hapa katikati lakini napenda kumshukuru Rais Mstaafu Mheshimiwa Jakaya Kikwete alipomsaidia Ray C, na ningependa Rais wetu wa sasa, Dkt. John Magufuli afanye hivyo ili tuweze kunyanyuka sisi tuliokwama,” ameeleza Saida.

Gabo amzungumzia Kanumba na Wema Sepetu

Msanii wa Filamu Tanzania, Gabo amesema si kweli tasnia ya filamu imeshuka baada ya kifo cha Steven Kanumba.

Muigizaji huyo ameeleza kuwa watu wengi wanaamini kutokuwepo kwa Kanumba kumedhoofisha soko la filamu za bongo movies ambae aliweza  kuleta changamoto ambazo kwa sasa hazipo.

“Sio kweli industry ipo vile vile, kwani jamaa alikuwa analeta changamoto kwa wacheza sinema wengi sana hivyo baada ya kuondoka ule ushindani ukawa umeshuka, hicho ndio kitu ambacho wanakikosa,” Gabo ameiambia Bongo Dot Home ya Times FM na kuongeza kuwa
“Lakini mimi nisema waendelee kuwa na mapenzi ya dhati ila wasisite kutoa malalamiko yao na kukosoa pale ambapo wanahisi pameenda tofauti kwa sababu changamoto za watu pekee ndio zinabadilisha.Tunajua hapo tunakosea inabidi tufanye hivi, kwa hiyo  tunabadilika kutokana na mawazo ya watu,” amesema Gabo.
Katika hatua nyingine Gabo amemuelezea muigizaji Wema Sepetu ni mtu wa namna gani katika ufanyaji kazi hasa pale walipokuwa wakishoot filamu yake mpya ‘Kisogo’.
“Ni dada mmoja ambaye yupo na utaratibu wake, ukiufuata na kuusikiliza utafanya nae kazi vizuri sana na atakuwa yupo poa sana. Ukiwa nje ya huo utaratibu unaweza kumuona ni msumbufu na ukamuona kero kwenye kazi,” ameeleza Gabo.

Thursday, June 22, 2017

Trump: Ukuta wa Mexico utakuwa na nishati ya jua

Rais wa Marekani Donald Trump amewaambia wafuasi wake kwamba pendekezo lake la ukuta katika mpaka na Mexico litakuwa na paneli za kunasa miale ya jua.
Akihutubia mkutano wa hadhara katika jimbo la Iowa, alisema kuwa paneli hizo za jua zitatoa kawi na kusaidia kulipia ujenzi wa ukuta huo wenye utata.



Alisema kuwa pendekezo hilo ni lake: Ni pendekezo zuri sio, hatahivyo paneli za jua zimeshirikishwa katika muundo wa ukuta huo uliowasilishwa na baadhi ya kampuni.
Wakati wa kampeni yake, bwana Trump aliahidi kujenga ukuta katika mpaka na Mexico ili kuzuia wahamiiaji haramu na ulanguzi wa dawa za kulevya.
Amesisitiza kuwa atailazimisha Mexico kulipia ujenzi huo , lakini rais wa taifa hilo Enrique Pena Nieto amepinga mpango huo.

Bwana Trump aliuambia umati uliomshangilia katika mkutano wa kampeni kwamba atatoa pendekezo ambalo hakuna mtu amewahi kulisikia.
''Tunafikiria kitu ambacho ni cha kipekee ,tunazungumzia kuhusu mpaka wa kusini, kuna jua jingi, na joto jingi pia''.

''Tunafikiria kujenga ukuta wa viage vya jua ambao utatengeza kawi na kujilipia. Njia hii Mexico italazimika kulipa fedha kidogo na hilo ni wazo zuri sio?''

Barakah The Prince: Sitaki kumpa mtu ‘kiki’

Barakah The Price ameamua kujibu mapigo baada ya Bright kuongea kuwa hajui kuandika mistari na amekuwa akirudia rudia maneno katika nyimbo zake

Akiongea kwenye E News ya EATV, Barakah amesema hawezi kuongelea lolote kuhusiana na hilo kwa kuwa hataki kuendelea kumpa kiki msanii mwenzake huyo ambaye alimshirikisha kwenye wimbo wa ‘Nitunzie’.
“Hiyo inaitwa unatafuta kiki kwa pikipiki, mimi siwezi kuongea nitakuwa nachafua brand yangu ya Rock Star na unajua mimi nikiongea watu wanazingatia sana, hivyo siwezi kuongelea watu kama hao katika interview zangu,” amesema msanii huyo.
Barakah ameongeza kwa kudai kuwa hamfahamu msanii anayeitwa Bright kwa kuwa anafanya kazi na wasanii wengi chipukizi.

Stars kukwea pipa leo kwa ajili ya COSAFA

Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kinatarajia kukwea pipa leo jioni kwenda Afrika Kusini kwaajili ya michuano ya COSAFA inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Juni 25 mwaka huu.

 Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kinatarajia kukwea pipa leo jioni kwenda Afrika Kusini kwaajili ya michuano ya COSAFA inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Juni 25 mwaka huu.

 Tumefanya mazoezi kuanzia jumatatu mpaka leo asubuhi, mazoezi ambayo kiujumla naweza kusema tumekwenda vizuri, kwa sababu vijana walifika wote siku ya Jumapili usiku, Jumatatu tukaanza mazoezi mpaka leo asubuhi.
“Afya za wachezaji zipo vizuri, tulipata tatizo kidogo kwa Shabani ambaye yeye alipata matatizo kidogo akiwa mazoezini lakini wachezaji waliosalia wapo katika kiwango kizuri.
“Tunategema kwa mazoezi tuliyoyafanya leo jioni tutafanya safari ya kwenda Afrika Kusini vizuri kwaajili ya mashindano ya COSAFA na kule tutapata nafasi ya kufanya mazoezi siku kama mbili Ijumaa na Jumamosi na tarehe 25 tutacheza mchezo wetu wa kwanza katika mashindano hayo ambayo tumealikwa na tukifanya vizuri tutaendelea tukifanya vibaya tutarejea kwaajili ya CHAN inayotarajiwa kuchezwa Julai 15 mwaka huu” amesema kocha mkuu wa Taifa Stars, Salum Mayanga.

Hata kama Ikulu hawajalipa bili ya maji, kata – Rais Magufuli

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ameagiza taasisi zote hata ziwe za serikali zisipolipa bili za maji zikatwe maji hata kama ni Ikulu.



Rais ameyasema hayo jana akiwa katika ziara yake ya siku tatu mkoani Pwani ambapo alizungumzia mradi wa maji na ulipaji katika taasisi zote.

“Mtu asipolipa bili, iwe taasisi yoyote hata kama ni Ikulu, narudia kusema kata.Kwa sababu tumezoa kudekezana, kwenye mawizara haya nafahamu, fedha za OC na hata fedha za bajeti wanazo, lakini suala la bili ya maji linakuwa si la lazima.”

Ujumbe wa Vanessa Mdee kwa Jux, atupa dongo gizani

Ni jambo zuri ukiona mtu wako wa karibu amefanikisha moja ya ndoto zake katika maisha yake. Ni muhimu kumpatia ujumbe ambao utakaomtia moyo katika kufanikisha mambo yake mengine aliyoyapangilia.

Vanessa Mdee ameamua kutumia vizuri fursa hiyo katika kumpongeza mpenzi wake Jux ambaye amehitimu masomo yake huko nchini China. Lakini katika ujumbe huo pia Vee amewapiga dongo watu waliokuwa wakimkejeli mwenza wake huyo kutokana na muimbaji huyo kutoonyesha picha yoyote akiwa na wanafunzi wenzake.
Kupitia mtandao wa Instagram, Vanessa ameandika:
Congratulations @juma_jux U finally done  and you done did it well. Hapo watu walikuwa wakiombaga picha za wewe darasani nadhani hii picha jibu la kutosha. Umeweza kufanya yote, MZIKI, BIASHARA NA SHULE… now that’s exceptional. Muda wa vibunda babaaa. Keep inspiring the YUTEEEEE