Thursday, June 8, 2017

Al Shabab lawaua zaidi ya wanajeshi 60 Somalia

Kundi la wapiganaji wa kiislamu wa Al -Shabab, linasema kuwa limewauwa askari 61 katika kambi moja ya kijeshi kaskazini mashariki mwa Bosaso nchini Somalia.

Idara ya BBC Monitoring, inanukuu vyanzo viwili vya habari kutoka kwa makundi yanayounga mkono Al-Shabab.

Kambi hiyo ya kijeshi ipo katika eneo la jimbo lililojitangazia uhuru wake la Puntland.
Mwaandishi mmoja pia wa VOA ameandika katika mtandao wake wa kijamii wa tweeter kuhusiana na shambulio hilo.

    Choose :
  • OR
  • To comment
No comments:
Write comments